Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia fursa hii na mimi nichangie hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana tukiwa ndani ya Bunge lako tukufu kipindi tunapitisha bajeti humu ndani kama hii Bajeti Kuu, nakumbuka makofi yaliyokuwa yanapigwa humu ndani kwamba bajeti hii haijawahi kutokea yaani haina mfano! Mwaka jana tukajenga hoja tukaonekana sisi kama vile mwaka jana hatueleweki. Sasa mwaka huu siku ya Alhamis wakati Waziri Mpango anawasilisha bajeti yake, nakumbukua maneno ya Spika mwishoni ana-windup anasema jamani haya ni mapendekezo ya bajeti, siyo bajeti haijawahi kutokea ni mapendekezo. Kwa sababu gani, kwa sababu yale yote waliyoyaahidi mwaka jana with confidence, hayajatekelezeka. Kwa kifupi kwa mara ya kwanza ukisoma hotuba yake yaani unaona kabisa ni bajeti ya kukiri kushindwa, bajeti ya kuomba msaada anaomba Simon wa Kirene kwenye bajeti aje ashuke, abebe msalaba wa zege humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma ukurasa wa 81 wametajwa viongozi humu ndani, mashuhuri. Alipowataja mimi nilikuwa nawakumbuka ikabidi nirudi tena nisome upya, ili niainishe hawa viongozi waliotajwa kwenye dunia, viongozi mashuhuri na uchumi wetu wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mtu wa kwanza aliyewekwa Deng Xiaoping, Rais wa Pili wa Jamhuri ya China, wakati anaingia madarakani alisema, to embrace people to be rich (kuwafanya wananchi kuwa mtajiri). To be rich is something to be glorious, Deng Xiaoping. Haya yapo kwenye hotuba ya Mheshimiwa Mpango haya kayasema, sasa tu- compare na kwetu, sisi tunataka watu wetu wawe matajiri? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kauli tumezisikia wote, tunataka matajiri waishi kama mashetani. Akatajwa Rais wa Pili, Lee Kuan Yew wa Singapore, huyu aliibadilisha Singapore kutoka dunia ya tatu kuwa dunia ya kwanza. Jambo la kwanza baada ya kupata madaraka, alifanya jambo moja, alisema lazima tuhakikishe watu wetu wanapata ajira (to promote stable employment jobs) kwa sababu Singapore unemployment ilikuwa iko juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo ya msingi ya kujifunza kwa huyu Rais wa Pili wa Korea, moja yeye ali- promote private sector, Singapore uchumi wake ni private sector. Sisi angalia private sector inavyolia leo, inalia siyo kawaida. Nenda kwenye mabenki angalia uchumi wake kule, mabenki yameporomoka, tumekaa na NBC wanakwambia imeshuka mpaka faida, dividend ya Serikali hakuna. Tumekaa na NMB, tumekaa na watu wa private sector wanailalamikia Serikali kwamba hatuwekezi kwa private sector. Haya aliyasema Rais wa Pili huyu ambaye amekuwa compared hapa, hizi sifa hizi yeye ali-promote private sector. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Lee alikuja Tanzania mwaka 1973 pale UDSM, miaka hiyo akina Mheshimiwa Chenge walikuwepo pale, akaja pale na Mwalimu Nyerere akamwambia Mwalimu hii sera yako ya ujamaa na kujitegemea njia hii siyo sawasawa, alizomewa kweli na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati huo. Alipozomewa akasema mimi nilichokisema ndiyo hiki, hii njia mliyochukua siyo sawasawa. Juzi nikamsikia Katibu Mkuu wako wa chama anasema turudi ujamaa na kujitegemea! Mnakotupeleka siko. Kama unatumia mifano ya watu ambao waliwajali watu wa chini kuinua uchumi halafu comparison how? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Dkt. Mahathir Mohamed wa Malaysia, unajua kabisa Malaysia imeendelea kwa mfumo wa PPP (Public Private Partnership). Haya tueleze sisi public private, tunasema reli tutajenga wenyewe, ndege tutanunua wenyewe, Stieglers’ Gorge tutanunua wenyewe, kwa nini, tutakopa, mwisho wa siku huu mfumo unaotumika sasa uko Tanzania tu. Duniani kote miradi mikubwa Serikali ina engage miradi mikubwa ya kiuchumi pamoja na private sector, lengo ili gharama zinazobakia, baadhi ya gharama ziende kusaidia wananchi. Sasa mikopo tunayochukua ni ipi, mikopo ya kibiashara na hii mikopo ya kibiashara tunayoichukua unajua maturity yake ni ndani ya muda mfupi miezi sita. Nilizungumza wakati wa Wizara ya Fedha kwamba, jambo la reli (standard gauge) siyo baya, lakini matokeo yake reli kabla haijaisha tunaanza kulipa mkopo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii nakueleza ukweli, Waziri wa Fedha asipodhibiti Deni la Taifa tunakwisha. Kwa sababu, mwisho wa siku angalia kwenye hotuba yake kwenye ule ukurasa ambao ameainisha ile bajeti yake nafikiri ni kama ukurasa wa 78, soma mapato anayoyapata. Mapato ya Serikali Kuu ya ndani anategemea kupata trilioni 20, lakini kwa miaka yote hawajawahi kuzidi trilioni 14, hapo ni kama amekusanya asilimia 100. Ukija ukiangalia kwenye matumizi, Deni la Taifa, trilioni 10, mishahara trilioni saba, matumizi mengineyo trilioni tatu, trilioni 20, hayo ni first and second charge, jukumu la kwanza na jukumu la pili, wana uhakika wa kukamilisha? Kuna miradi ya maendeleo, hakuna? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana ukipitia bajeti nzima mwaka huu trilioni 10 hawajakusanya, miradi ya maendeleo haijafanyika, Halmashauri zina-suffocate! Haya tunawaambia kwa nia njema. Sasa unamgusa mtu kama Nelson Mandela amekaa jela miaka 27, mtu wa kwanza, hebu fikiria mtu aliyekufunga ndiyo unamuweka kuwa Makamu wako wa Rais, Frederik Willem de Klerk. Halafu yule aliyekuwa anamtesa Mandela ndiyo alikuwa bodyguard wake mpaka anakwenda kabirini, ndiyo alikuwa Chief bodyguard, yule gerezani aliyekuwa anamtesa miaka 27, anayemfanyisha Mandela kazi ngumu mpaka akaumwa TB ndio alikuwa bodyguard wa Mandela. Niambie wa kwetu angefungwa hata miezi sita ingekuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati fulani mnakimbia vitu. Hebu kwa mfano unataka umuige Mandela, tumekuletea hotuba ya kurasa 521 unakimbia hotuba, mtaweza tabia za Mandela? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unajua wakati mwingine kama unakimbia maoni halafu unataka kuwa Mandela, hizi ndio tunaita nadharia. Utekelezaji ni tofauti na nadharia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwalimu Nyerere huyu sifa zake hazielezeki, ana sifa kweli na mimi ninakiri kwamba Mwalimu Nyerere anapaswa kuwa Mwenye Heri kama Kanisa Katoliki wanavyotaka, kwa sababu gani, aliunganisha Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, akina Mtei wale wa Kaskazini walikuwa Magavana wake. Watu wale wa Usalama wa Taifa, Mkuu wa Usalama walikuwa ndiyo watu wake waliokuwa wanamsaidia, akina Ndugu Kombe wale na akina nani, leo huwezi kusema Taifa moja la upande huu, sijui Kaskazini wasubiri, hawa hivi, haiwezekani!

Mheshimiwa Naibu Spika, it is ok. Sina shida na suala la ETS, mkitaka kushughulika nendeni mpaka kwenye simenti, sigara na mafuta.