Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nikushukuru kwa kunipa nafasi, nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na wataalam wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa maslahi ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipongeze mwongozo wa Mheshimiwa Rais kwa kuongoza nchi iwe na mwelekeo wa viwanda, iwe na mwelekeo wa kizalendo kwa watu wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina-introduce Electronic Tax Stamp (ETS) ni jambo ambalo zuri sana na ukitizama tumechelewa, lakini uhakika wa source ya revenue ya Serikali utapatikana kwa utaratibu wa mfumo huu wa Electronic Tax System (ETS). Lakini nilitaka kujiridhisha tu au Serikali imejiridhisha vipi na huyu aliyepewa kazi hii, due diligence ilifanywa na nani? Kwenye semina tumeambiwa wamefanya Mabalozi, lakini ukitizama taarifa mbalimbali, hii kampuni ina matatizo makubwa. Hii kampuni ina kesi Morocco, wamefanya price offering mara kumi zaidi ya nchi zingine walizofanya kazi hii. Kampuni hii inachunguzwa na Bunge la Kenya, kwa malpractice. Kampuni hii imeziangusha Serikali zingine kutokana na mfumo wake wa malpractice na corruption. Sasa Mabalozi hawa waliofanya due diligence ya kampuni hii, mimi nitapenda waitwe waje waulizwe taarifa zao walizipata wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanya semina; TRA na Wabunge na hoja zilizoulizwa na Wabunge kwenye semina Serikali walizi-defer, walishindwa kuzijibu. Kutokana na hoja za msingi za kizalendo ambazo Wabunge wameuliza.

Mheshimiwa Naibu Spika, TTCL chombo cha umma, kwa gharama za mradi huu wa bilioni 48, mimi binafsi naomba Serikali i-revisit mpango wake wa kuajiri watu wa nje kusimamia makusanyo ya kodi nchini Tanzania. Unapo- surrender sovereign ya tax regime ya nchi kwa kampuni ambayo tayari ina matatizo makubwa kama haya duniani na sever ya kampuni hii ni mali ya vendor mwenyewe. Naiomba Serikali tena na nia njema ku-support mpango huu wa ETS, lakini bado ningeomba shughuli hii ifanywe na TTCL ambacho kina uwezo, chombo cha umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unaposema information za vendor huyu zitakwenda kwenye data center, kuna njia nyingi sana za ku-under declare traffic kwenda kwenye data center ya Serikali. Kuna command nyingi sana za mitandao unaweza uka-hide information zingine. Kwa hiyo, mpango huu ni mzuri naunga mkono asilimia 100, lakini naomba Serikali i-revisit jambo la ku-surrender regime ya tax kwa Kampuni ya nje ambayo tayari ina misuguano kwenye nchi nyingi sana. Kwa hiyo, naomba kazihii nzuri, ni muhimu kwa Taifa letu lakini wapewe TTCL.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2008 tulishauri Serikali kuhusu masuala ya wizi wa declaration za traffic kwenye mitandao ya simu. Serikali ikanunua mtambo, walituambia walinunua mwaka 2008 kumbe hawakununua, walimuweka Mwekezaji ambaye kaja na mtambo wake wa gharama za 50 billion wakaingia mkataba wa miaka 15, which was very wrong. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, masuala ya mitandao server kama ni mali ya vendor utapigwa tu na tumepigwa na tunaendelea kupigwa. Kwa hiyo, hoja yangu tulihoji hata gharama ya mtambo wenyewe na huu mkataba kwenye semina tumeambiwa ni miaka mitano. Miaka mitano mtu anasimamia sovereign ya regime ya kodi nchini na hakuna popote ambapo tumepewa comfort ya forensic audit ya mtambo wake atafanya nani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna nchi nyingi wameweka hii system, kuna kitu kinaitwa new generation quickly response, hoja kubwa ni makusanyo lakini ku-cub na kuzuia elicit goods katika soko ambalo ni jambo zuri sana. Mitambo hii inayowekwa sasa hivi huu sijui, kwa new generation mimi na wewe ukienda dukani unatumia app yako ya simu kuweza kuona stamp ile na goods ambazo ziko mitaani ni genuine. Sababu stamp za mitaani ambazo siyo genuine hazitakosa ku-have return ili kuthibitisha unatumia simu yako una-log kwenye ile code ya stamp inakwambia hii ni genuine au siyo genuine. Sasa tulitaka kujiuliza mtambo huu ambao Serikali wanatuambia walishainigia mkataba unayo app kama hii ambayo kujiridhisha mfanyabiashara, consumer kuweza kujua hii stamp iliyowekwa hapa ni kweli stamp ya Serikali na mwananchi wa kawaida anaisaidia Serikali kwa kwenda katika maduka au katika supermarket aki-log in pale pale na simu yake na yeye anapewa majibu kuwa hii ni stamp ya Serikali au ni stamp ya mitaani, nilitaka kujua hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, server inapokuwa ni mali ya vendor si rahisi kwa TRA au Serikali kujua under declaration ya ripoti yoyote ya vendor, siyo rahisi. Kwa hiyo, nilikuwa naomba, naunga mkono mpango huu naunga sana 100 percent. Ombi langu uwekezaji huu ni mdogo sana,
tuiwezeshe TTCL ifanye hii kazi siyo chombo kutoka nje.
(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Bombardier mpya zinatolewa Q400 New Generations, abiria 96 (96 passengers) flies Dar es Salaam - Dodoma siku zote watu wanakosa nafasi. Huduma nzuri, performance nzuri, tukipata Bombardier Q400 New Generations ya abiria 96 gharama za uendeshaji zitashuka, tutakuwa na abiria wengi kwenye ndege. Kwa hiyo naomba Waziri wa Fedha hili nalo alitizime, kuweza kununua New Generation Bombardier Q400 ili tuweze kupunguza gharama za uendeshaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na Taarifa ya Kamati ukurasa wa 47 chombo hiki kiendeshwe na mamlaka ya umma ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono.