Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima kubwa napenda nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara, kwa kazi kubwa wanayofanya ya kupambana na changamoto mbalimbali za Kilimo, Ufugaji pamoja na Uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utajikita katika mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Ufugaji; katika Mkoa wa Dar es Salaam, ufugaji mkubwa unaoendelea ni ufugaji wa kuku wa nyama na mayai. Changamoto kubwa tuliyonayo ni upandaji holela wa bei za madawa na chakula cha kuku. Naiomba Serikali iangalie jinsi gani ya kudhibiti upandishaji bei za madawa ya mifugo.
Watanzania walio wengi wamejiajiri wenyewe kwa kuvua na kufuga kuku wa nyama lakini kadri siku zinavyozidi kuendelea utakuta kwenye supermarkets kumejaa kuku wa kutoka nje na samaki wengi kutoka nchi za nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, uvuvi haramu; napongeza juhudi za Serikali jinsi inavyojitahidi katika kupambana na uvuvi haramu pamoja na juhudi za Serikali bado wapo. Ni vema Serikali ikaongeza juhudi zake kwenye kudhibiti uvuvi huo haramu ambao ni hatari sana kwa uvuvi endelevu wenye tija kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo; nitachangia juu ya kilimo cha mbogamboga na matunda. Kilimo cha mbogamboga na matunda kinachoendelea Dar es Salaam hatuna msaada wowote wa Serikali katika uboreshaji wa kilimo hiki. Tunakiri wako Maafisa Kilimo lakini utendaji wao ni mgumu kulingana na mazingira, pia ufuatiliaji wao ni mdogo. Wananchi wanajilimia wenyewe kama hakuna Wataalam. Je, wataalam hao wanafanya kazi gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa Kilimo wako kila Kata, naomba Serikali na Wizara ya Kilimo kukaa na TAMISEMI kuangalia utendaji wa kazi wa Maafisa hao. Mkoa wa Dar es Salaam hatupati unafuu wa pembejeo za kilimo. Mbogamboga ndiyo chakula cha Watanzania walio wengi katika Jiji la Dar es Salaam. Je, Serikali imetuletea mpango gani katika Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam katika kuboresha Kilimo cha mbogamboga na matunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kukosa soko la mayai; Mkoa wangu una tatizo kubwa la kukosekana kwa soko la mayai. Maeneo ya Kitunda, Chanika, Kibamba, Mbagala, Mbande, Somangira, Gezaulole, Pemba Mnazi na Kisarawe II. Kata zote hizo kuna wafugaji wazuri lakini inafika kipindi soko la mayai linaanguka na wafugaji kukosa mitaji kwa kuwa wanafanya biashara kwa hasara.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.