Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, Rungwe Mashariki ni moja kati ya Miji inayozalisha mazao mengi ya chakula na biashara, lakini tumekuwa na tatizo la masoko na kupelekea mkulima kupata kipato kidogo na kibaya zaidi wanaofaidika ni Madalali ambao wanachukua pesa nyingi kuliko mkulima mwenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, maoni yangu; tujengewe soko kuu la mazao haya ya ndizi na chai, kwenye chai mkulima ananyonywa kwa kupangiwa bei hasa kwa kutokana na kutokuwa na ushindani katika soko.
Mheshimiwa Naibu Spika, mbolea imekuwa tatizo kubwa hasa mawakala wengi sio waaminifu na kupandisha bei mazao kama kahawa yalikwisha kwa kukosa motisha kwa wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, mageti ya mazao ni kikwazo kikubwa kwa wakulima wadogo kwani tozo zimekuwa kubwa sana zisizo na ulinganifu katika utozaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, uvuvi katika Ziwa Nyasa unatoa samaki bora sana ambao ni kivutio cha walaji wengi. Ningependekeza Wilaya ya Kyela itengewa pesa ya kutosha juu ya utunzaji wa mazalia ya samaki na kuongeza uzalishaji na kutoa ajira kwa vijana wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, zao la maziwa; Wilaya ya Rungwe ina mazao ya maziwa kwa wingi, ni lini Wizara itasaidia upatikanaji wa viwanda vidogo vya kusindika mazao haya ili kuongeza thamani ya mazao haya na kupata faida katika mapato ya Halmashauri na ya mmoja mmoja katika jamii.