Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa leo nimevaa vazi adhimu la Kiislam na pengine nitasema maneno makali kidogo naomba nianze kwa Sala “Audhubillah mina-Shaitwani Rajeem, Bismillah Rahmani Raheem”

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Mpango na Naibu wake na watu wote wanaomsaidia kwenye Ofisi yake. Naomba niseme kwa hisia zangu kwamba yeye ni Waziri wa kwanza toka Serikali zote zianze, Waziri ambaye anapambana na Watanzania kuwabadilisha kuwatoa kwenye kukwepa kodi, kuwapeleka kwenye kulipa kodi. Kwa hiyo, nimwombe na nimshauri asikate tamaa, hii mishale anayopigwa ni moja ya maboresho lakini kazi yake hata Wapinzani wanajua anafanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nimshauri Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango, nianze na biashara ya dhahabu. Biashara ya dhahabu ameweka kodi ya asilimia 14 ukichukua makorokoro kuanzia kuchimba mpaka kuuza. Kodi hiyo hiyo anatozwa anayechimba gramu moja, anatozwa na mtu mkubwa kama GGM kodi moja. Ukija kuchunguza wale ambao wanachimba kwa kiasi kidogo, wachimbaji wadogo ni kama wanamtumikia tu yule mkubwa apate faida, sisi tuendele kupata hasara.

Mheshimiwa Spika, tulishawahi kushauri mara nyingi Mheshimiwa Waziri kwamba ukienda nchi kama Uganda wao wana-charge 0.5 kwa wachimbaji wadogo, ukienda Rwanda 0.6, ukija Tanzania 14. Kwa nini Mheshimiwa Waziri asiondoe kodi kwa wachimbaji wadogo ikawa hata zero ili tukapate dhahabu nyingi kwa sababu kui-control dhahabu ni kazi ngumu, dhahabu wengine tunaiokota mashambani, ataidhibiti vipi?

Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri kwa nini asiondoe kodi huku kwa wachimbaji wadogo ikawa zero tuwavutie na wengine wauze Tanzania ili sisi tupate tu asilimia moja kwenye export. Mtu anayesafirisha ndiyo amlipe lakini kwa kodi asilimia 14 dhahabu ya milioni 100 unaweza ukapata faida ya milioni 2,500,000, unataka mimi nikalipe bei gani? Lazima nikwepe. Kwa hiyo, nimshauri sana Mheshimiwa Dkt. Mpango aliangalie hilo.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusiana na mikopo ya halmashauri, nilikuwa napiga hesabu kwenye halmashauri yangu ni kama Mbunge wa nane. Ukipiga hesabu ya ambazo tumekopesha tuna karibu bilioni mbili toka tuanze Ubunge pale, lakini hizi hela hazina ufuatiliaji. Kwa nini Mheshimiwa Dkt. Mpango Waziri asizigeuze hizi halmashauri zikawa na Taasisi, tunapokopesha zile hela tuwe na taasisi kabisa, tuna karibu bilioni mbili Geita, ingekuwa ni benki tayari iliyokuwa na sifa ya kukopesha ikawa na commitment ya kuwadai wakulima, lakini sasa kila mwaka tunakopesha, hakuna mtu anayedai, tukikopesha hela hakuna mtu anayedai, pesa zinakwenda na hazina mfuatiliaji. Ukimweka Afisa Ushirika kufuatilia akienda kule na yeye anaomba kuku tu na mkaa. Kwa hiyo, nashauri tujaribu kubadilisha taswira hii tuangalie kama hizi halmashauri tunaweza tukazigeuza zikawa ule mkopo wake tunaotoa kwa wakulima kuwe na Taasisi ya kuweza kudai kabisa zile pesa na yenye commitment na kazi hiyo peke yake.

Mheshimiwa Spika, suala lingine Mheshimiwa Dkt. Mpango; naona kuna Benki ya Wakulima, ndugu zangu Wabunge hii Benki ya Wakulima tunawapelekea matapeli tu, hakuna mkulima ana-qualify kukopa kwenye zile Benki hayupo, wala mkulima wa kijijini hahitaji kukopa bilioni moja sana sana wanakopa laki mbili, hakuna sifa za kuwakopesha wakulima na ndiyo maana nikaona tujaribu kubadilisha haya mazingira tuwe na benki zinazoendeshwa na halmashauri zenyewe kutokana na hizi pesa tulizokwishazikopesha.

Mheshimiwa Spika, lingine, ni suala la makinikia, wazo la Serikali ni zuri sana, kwanza sisi tunaotoka kwenye dhahabu tunaona kama ni neema Mungu ametuletea, lakini naomba nishauri mfanyabiashara wa Tanzania siyo adui na sisi tumo humu kwa ajili ya kutetea watu wetu.

Mheshimiwa Spika, niliona Mheshimiwa Waziri wa Madini alitoa kauli akasema “kuanzia kesho hakuna kusafirisha carbon”, Mheshimiwa Waziri anaongoza Taasisi za fedha; hawa walio na illusion plant kule kijijini, kule Mwanza na sehemu zingine, nataka niseme hapa kama yuko mtu atanibishia wote ni darasa la saba, lakini wamekopa benki na benki zinataka marejesho ukiawaambia leo wote mrudi Geita wengine Singida kuna changamoto. Mwingine unakuta siku hiyo ndiyo mwezi wake wa kulipa marejesho, carbon imezuiwa kusafiri.

Mheshimiwa Spika, mwingine amekopeshwa na yule aliye na illusion kule Mwanza, jinsi ya kukusanya ile hela ni kazi, hata unapomwambia kesho arudi kule anapokwenda tena mfano mmoja tu ni Geita; maeneo wanayopewa wale wenye plant kuhamisha kujenga hakuna umeme, hakuna barabara, inachukua miezi miwili. Mtu anapigwa interest za benki, kwanini tunawaona wafanyabiashara kama maadui?

Mheshimiwa Spika, nimshauri Mheshimiwa Dkt. Mpango, maamuzi mengine haya tuwe tunayapa muda, mimi sikatai wazo na watu tumelipokea vizuri, lakini tungesema basi kwamba tunawapa siku 60 au 40 ili muweze kujiandaa kuhamisha mashine zenu hakuna mtu ambaye angelalamika kwa sababu hata wakati wanakwenda kujenga huko walikokuwa ni Taasisi za Serikali zilitoa vibali na kukubali watu wawekeze, kwa nini tunakuwa tuna vigeugeu?

Mheshimiwa Spika, suala lingine, mara nyingi najiita Chief watu wanadharau, haya maneno yaliyotokea jana nilizungumza mwanzo kwamba mimi na abiria wangu tulikamatwa na samaki piece tatu, kwenye basi tukaombwa ruler, hamkujua? Sasa jana ruler Bungeni, lakini niseme tu ukweli kutoka moyoni mimi kama Chief kwa mara ya kwanza leo nimeamini Wagogo, watani zangu kumbe wana akili kubwa sana. Ulichokifanya Mheshimiwa Spika kusamehe na kusema ukichukizwa unasamehe Waziri ajitafakari! Hilo ni neno kubwa bora hata ungechukua hatua nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hilo neno la kwamba mtu amekuudhi kwa hatua ile halafu unakaa kimya, Wizara hii tumekuwa na Mawaziri nakumbuka watano tena wote Madokta, Mheshimiwa Rais wangu, Dkt. Magufuli, Dkt. Mathayo, Dkt. Kamani, Dkt. Tizeba wote hawa walifanya kazi yao nzuri na uvuvi haramu walikuwa wanapambana nao kwa style yao kama viongozi, leo tumeleta Mgambo sijui shule za design gani hizikila siku huwa nashangaa, lazima tufike mahali tuchukie. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, huwa nasema kila siku ni vizuri tukakaguliwa vyeti, watu wana elimu za kuunga unga unamkabidhi Taifa kama hili tutakufa. Sasa hebu jiulize, yeye mwenyewe anakiri anasema mimi niliamua kuwaita ili tutekeleze zoezi la operation, yeye ndiyo mtunga sheria? Hajui Sheria za Bunge jinsi ya ku-arrest Bunge? Anazijua kabisa anaamua kukiuka kwa kutafuta kick na huu Urais utakuja kuwatokea puani. Hata sisi Wasukuma tumelia na tumelalamika tulipokosa msaada, tumefanya ulichokifanya wewe. Tumeamua kunyamaza na kumuachia Mungu apambane naye. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.