Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Awali ya yote nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kumaliza mwezi Mtukufu wa Ramadhan na sasa tumeanza mwezi wa Shawali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kukushukuru wewe na kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa ushirikiano mlionipa wakati nilivyopata msiba, nawashukuru sana na nathamini support yenu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa maneno yafuatayo; Taifa lolote linapopanga bajeti linatengeneza instrument ambazo zitatumika kuisaidia bajeti hiyo kuweza kutekelezwa na wakati huo huo kuchochea uzalishaji na kuisaidia Serikali kukusanya kodi yake. Kwa dhati kabisa, ni mara chache sana nimempongeza Waziri wa Fedha na mimi kwa dhati kabisa safari hii nimpongeze kwa measures alizochukua kwenye fiscal hasa za kikodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatua ya kwanza aliyoifanya ya kikodi ni maamuzi ya Waziri wa Fedha kutoa amnesty ya kipindi cha miezi sita kwa watu wanaodaiwa kodi, riba na penalties kwa wafanyabiashara, hii ni taswira njema. Wafanyabiashara wengi wamekuwa na malimbikizo na kumekuwa na kesi nyingi za kikodi katika Tax Tribunal ambazo wengi wanapambana na Serikali kupinga either penalty ama interest, Waziri ametoa amnesty, kwamba watu wanaodaiwa kodi anawasamehe riba na penalty kwa kipindi cha miezi sita.

Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri utakapokuja kufanya wind-up naomba atoe flexibility ya kumpa Commissioner General wa TRA kwa sababu ndiye yaliye kwenye daily operations aangalie pale ambapo mtu anapokuja na payment plan, either ni ya mwaka mmoja, inategemea anadaiwa shilingi ngapi ili waweze kumpa hiyo amnesty isiwe restricted ndani ya kipindi cha miezi sita.

Mheshimiwa Spika, yeye mwenyewe anafahamu TRA inadaiwa na wafanyabiashara hawana haki ya kudai interests, hawana haki ya kukupiga penalty. Kwa hiyo kama wanavyosema Wazungu, scratch my back I scratch yours, ameonesha good gesture, nakuomba u-extend hii amnesty ili Mtendaji Mkuu wa TRA aweze kufanya maamuzi kutokana na hali halisi ya mfanyabiashara huyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo nataka niseme, wafanyabiashara na it is natural, kutumia loopholes za kisheria kutokulipa kodi na hii siyo dhambi na Serikali inafanya jitihada ya kuboresha sheria zake. Waziri amekuja na Mfumo wa ETS. Moja ya maeneo ambayo wafanyabiashara hutumia nafasi ya ku-avoid kodi ni kwenye VAT. Eneo hili liko connected na production.

Mheshimiwa Spika, nimesikia mawazo ya Waheshimiwa Wabunge, nami nataka nimwombe Waziri, cautions zote zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge juu ya mambo haya, juu ya hii Kampuni inayoitwa SCIPA, zifanyie kazi. Hata hivyo, practice na studies zinaonesha maeneo ambayo hii Kampuni ya SCIPA imewahi kufanya kazi kumekuwa na positive result.

Mheshimiwa Spika, pale ambapo tunajua kwamba wana kesi Morocco ama wamekuwa wana tuhuma ya rushwa, suala la rushwa ni suala la watu. Kama mfumo utaruhusu watoe rushwa ili waweze ku-yield more, it is our weakness, lakini kama mfumo wao huu utatusaidia kufanya production count, kama mfumo wao huu utatuongezea mapato; nimwombe Mheshimiwa Waziri tunapokuja mwaka kesho ambapo atakuwa na miezi sita ya utekelezaji wa bajeti atuletee taarifa ya performance ya hii kampuni, imetuongezea mapato kwa kiwango gani na kama haijatuongezea mapato aweze kuchukua hatua stahiki.

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuwa na hofu kwa sababu let us accept the reality, wao wana patent right, wao ndio wana teknolojia, sisi tunahitaji huduma yao; tuhofie kwa sababu walitoa rushwa nchi fulani? Kama waliwapa watu rushwa it is their problem na sisi watu wetu wakipewa rushwa it is our problem. Sisi tunahitaji huduma tuangalie mechanism ambayo we can yield more kwa mfumo huu.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka kuongea, ukisoma taarifa hii ya uchumi ya Wizara ya Fedha kuanzia ukurasa wa nne mpaka wa saba, Waziri kaonesha key economic indicators ambapo jibu la failure zote hizi tulizozitaja ni sekta mbili; sekta ya kilimo na ya mifugo. Waziri ameonesha uzalishaji wa viwandani umeshuka kutoka asilimia 7.8 mpaka 7.1; biashara imeshuka kutoka asilimia 6.7 mpaka 6; malazi na huduma za chakula kwa maana ya hoteli na akinamama ntilie imeshuka kutoka 3.7 mpaka 3.2; shughuli za fedha na bima zimeshuka kutoka 10.7 mpaka 1.9; na hii ni analysis ya 2016/2017, ni taarifa ya hali ya uchumi. Shughuli za sanaa zimeshuka kutoka asilimia 8.6 mpaka asilimia 7.6; shughuli za kaya binafsi (household activities) kwa maana ya kuajiri wafanyakazi wa ndani, walinzi na nini zimeshuka kutoka asilimia tatu mpaka 2.7.

Mheshimiwa Spika, hizi indications zote ukienda kwenye mapato ya Serikali tuna-project kupungua kwa mapato yetu ya ndani kwa asilimia 10. Tafsiri yake ni moja tu, kwamba purchasing power ya watu wetu kwa ajili ya kununua bidhaa, kufanya shughuli za kibiashara, zimeshuka.

Mheshimiwa Spika, sasa what is the solution? Nami nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Mpango, kwa mara ya kwanza priority yake ya bajeti ya mwaka huu ni kilimo, kwa mara ya kwanza. Solution ni ku-invest kwenye agriculture. Waziri kwenye tax measures alizoweka safari hii ametoa corporate tax incentive ya 20 percent kwenye viwanda vinavyozalisha mazao ya mifugo kwa maana ya leather sector na dawa lakini ni viwanda vipya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuna viwanda saba katika nchi yetu vinavyozalisha mazao ya ngozi na viwanda hivi havifanyi vizuri. Kwa nini; sababu kubwa ni mbili. Sababu ya kwanza ni export levy ya 10 percent, kwamba Mtanzania aki-process wet blue ndani ya nchi yetu kuiuza nje anachajiwa export levy ya 10 percent, kwa nini? Wakati competitors wote, kwa maana ya ukanda wetu wa Afrika Mashariki hawachajiwi 10 percent ya export levy. Ushauri wangu kwa Waziri wa Fedha; tufute 10% ya export levy kwenye wet blue.

Mheshimiwa Spika, ushauri wa pili kwenye Sekta ya Leather; sisi tumeweka 80 percent ya kodi kwa ajili ya ku- export raw, lakini unapoweka export levy ya 80 percent kinachotokea katika maeneo yetu ni jambo moja; bei ya raw nje ni nzuri, kwa hiyo wanachokifanya wafanyabiashara na Wizara ya Fedha inajua na TRA inajua; wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu wanachukua ngozi zetu raw kwenye container ya 40 feet wanaweka just 10 percent ya wet blue wana-declare ni wet blue wakati wame-export raw, matokeo yake Serikali inakosa.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu katika hili; ban export ya raw, aite viwanda vilivyopo vinavyozalisha ngozi ndani ya nchi yetu; na Mheshimiwa Waziri Mwijage anavijua, a-sign nao performance agreement, aondoe export levy ya 10 percent, ban export ya raw. Tunazalisha vipisi milioni nne. Kuna kiwanda kimekuja Tanzania kutoka Ethiopia, ni Wachina, wameweka investment yao pale kwenye EPZA Bagamoyo, wanaomba leo kupewa haki ya ku-import ngozi raw kutoka Ethiopia kwa sababu wao uzalishaji wao kwa siku ni vipisi 30,000, hawavipati ndani ya soko letu because of smuggling. Kwa hiyo ushauri wangu; ili tuweze ku-create value kwenye mazao ya mifugo, achukue hatua hizi mbili.

Mheshimiwa Spika, nimeona ametoa exemption ya VAT kwenye mashudu ya soya; hatukamui soya, sisi tunakamua alizeti, tunakamua pamba, aweke VAT exemption kwenye mazao ya pamba, kitatokea nini? Mifugo yetu na kwenye taarifa hii ya hali ya uchumi uzalishaji wa nyama na consumption ya nyama imeshuka kwa asilimia 14. Ushauri wangu huu ni kwamba Watanzania wataingia kwenye feedlotting.

Mheshimiwa Spika, leo ili uweze kumchinja ng’ombe, hawa ng’ombe wetu wa Kisukuma, Kigogo na Kinyaturu, ili umchinje uuze nyama yake technically anatakiwa achinjwe ng’ombe mwenye miezi 18 maximum miezi 20. Hatuwezi kwa sababu the cost of feedlotting ni kubwa mno. Mashudu ukinunua yana VAT, kwa hiyo ili tuweze ku-create proper value chain kwenye sekta ya mifugo nashauri create an exemption ya VAT kwenye mashudu kwa sababu kinachotokea sasa hivi mashudu yako yote unayozalisha ndani yanapelekwa Kenya, kwa sababu yana exemption kwao yanarudi ndani sisi tunageuka soko kwa raw material ya kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka niishauri Serikali, Wizara imechukua hatua na ni muhimu Mheshimiwa Waziri wa Fedha, kama hatutachochea ufanyaji biashara katika uchumi wetu, mwaka kesho atakuja hapa hajafikia target ya makusanyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hali ya benki zetu, non-performing loans Serikali imechukua measures ambazo mimi kwa kweli naziita cosmetic, samahani akinamama; kwamba mama amekaa kwenye dressing table anachukua poda anaweka haibadilishi alivyo naturally. Cosmetic measures tulizochukua ni nini; BOT imeamua kupunguza some of the regulations zake za deposits na non-performing loans.

Mheshimiwa Spika, lakini unawapa watu extention ya miezi mitatu ambao wameshindwa kulipa mkopo. Wameshindwa kulipa mkopo kwa sababu gani; kwa sababu wameshindwa kufanya biashara. Kwa hiyo ni wajibu wa Wizara ya Fedha kuhakikisha kwamba tunachochea trading na ili tuchochee trading ni lazima tuchochee Sekta ya Kilimo. Kama kwenye kilimo hatutaamua kuanzisha price stabilization; wakulima wetu wanazalisha mahindi, kuzalisha kilo moja ya mahindi; narudia, ni Sh.357.

Mheshimiwa Spika, leo kilo moja ni Sh.150 au Sh.200, mkulima anapata hasara. Ni wajibu wa Wizara ya Fedha kwa kutumia vehicles tulizonazo ambayo moja ni Bodi ya Mazao Mchanganyiko na nyingine ni NFRA. Tuwape fedha wanunue haya mahindi kwa competitive rate kutoka sokoni halafu tuyatafutie soko wauze, kwa sababu hii fedha ni revolving. Nafahamu hofu ya Wizara ya Fedha, imekuwa kwamba wakitoa fedha kwenda NFRA huwa hairudi. Sasa ni udhaifu wetu sisi, kwamba mkulima kazalisha mahindi hana soko, tutachochea vipi biashara? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo kule kwetu Nzega; natolea mfano kwangu Nzega; leo mkulima amelima mazao yake, amevuna anataka kuuza, tunatumia mifumo tuliyonayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, leo kule Nzega wafanyabiashara wa mazao wanakuwa disturbed. Tumeleta vi-regulation kwamba eti mpunga usiweke kilo 90 kwenye gunia, ukikutwa unaweka faini. Waganda wanaokuja kununua mchele Nzega wanakuwa disturbed, wanahojiwa, kiko wapi kibali
cha kuja kununua mashineni, huna kibali faini 500,000. Tunawanyima fursa wakulima wetu kuuza mazao yao, matokeo yake hawawezi kubadilisha maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwombe Waziri, kachukua measures nzuri lakini kama hataweka jitihada kwenye sekta ya kilimo na mifugo mwaka kesho tutakuja hapa hatujafikia malengo ya bajeti tuliyotarajia.

Mheshimiwa Spika, nashukuru na naunga mkono hoja.