Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nipo concerned sana na dhamira ya Serikali ya kujenga uchumi wa viwanda kutokana na uzito mdogo unaopewa sekta zinazohusisha Watanzania wengi takriban asilimia 70 au zaidi. Kiasi kidogo sana cha fedha zilikuwa zikitengwa miaka ya nyuma, lakini hata hivyo zilizotolewa ni takriban asilimia 50 au chini.
Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 0.92 ndiyo imetengwa kwa ajili ya sekta ya kilimo kwa bajeti ya 2016/2017. Azimio la Maputo la kutenga asilimia 10 ya bajeti kwa ajili ya kilimo tutafika kweli kwa utaratibu huu? Ili uchumi wa viwanda tuweze kuwa nao, kama kweli hiyo ndiyo dhamira ya Serikali ni lazima tuoneshe kwa vitendo kwa kutenga bajeti ambayo itawagusa kiuchumi wananchi waliopo kwenye bottom of pyramid ya rasilimali watu na hawa ni wakulima, wafugaji na wavuvi kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mara ya kwanza na kwa kutumia bajeti ya kilimo kama kielelezo, naona malengo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano tumeanza vibaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, bilioni 100 kila mwaka kwenda TADB lazima zitengwe na zielekezwe kwenye kukopesha SME’s na ikiwezekana kwenye uwekezaji mnaongeza mnyororo wa thamani. Ila katika hili sijaona mpango mkakati wa SME development strategy inayolenga kukuza SME’s zinazojikita kwenye kilimo na mifugo – value chain. Ni lazima Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano unyambulishwe kwenye annual spectral budgets kama nilivyoeleza hapo juu, lakini kwenye hili mpango unaenda Kaskazini na bajeti ya sekta kipaumbele inaenda Kusini. Hatutafika kwa style hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono.