Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami nipate kutoa mchango wangu na naomba Serikali haya nitakayoyasema pia wayachukue.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuna vitu ambavyo hatuangalii. Ulinzi ni jambo muhimu sana katika Taifa hili, lakini tumekuwa tunatenga bajeti hewa, kwa nini nasema hivyo? Mwaka wa fedha 2016/2017 zilitengwa bilioni nane na pesa hizi zilitengwa kwa ajili ya uwanja wa ndege, kukarabati maghala ya silaha, lakini fedha hizi hazikuenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gongo la Mboto paliwahi kutokea maafa makubwa tu. Ndani ya vyombo hivi vya ulinzi na usalama, hasa Jeshi la Wananchi kuna vitu ambavyo ni nyeti ambavyo vinatakiwa Bajeti ya Serikali ipelekwe kwa wakati muafaka. Sasa vitu kama hivi tunapitisha ndani ya Bajeti ya Serikali halafu havitekelezeki tunasema ni bajeti hewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija kwenye suala la wastaafu, Wanajeshi wastaafu siyo watu wazima sana, ustaafu unajua kuna wastaafu wengine ambao pia wameshafika umri wa kustaafu lakini mpaka sasa hivi wengine wako kazini, lakini hawa walishastaafu. Ni kwa nini hawataki kuwapa stahiki zao Wanajeshi wastaafu? Wanajeshi Wastaafu sasa watajisikia unyonge na ni watu na taaluma yao, wamekusudia vipi kujenga mioyo yao au wanataka ibadilike. Kwa sababu ni watu wenye fani mbalimbali lakini Serikali haitaki kutoa mafao yao kwa wakati. Siyo Wanajeshi tu, wapo wastaafu wengi ambao wanaidai Serikali, je, mpaka sasa hivi Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wastaafu wote inawalipa kwa wakati muafaka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna Wajane. Hawa Wanajeshi ambao wanakwenda kupigana huko nchi za wenzetu wanakwenda kulinda amani, lakini wengine wanapata maafa, wengine wanakufa, hata hapa kwenye nchi yetu, lakini hawa Wanajeshi wakishakufa hawa wajane hawaangaliwi, wala zile stahiki zao hawapewi kwa wakati muafaka. Ni lini Serikali watatoa hizi stahiki za hawa Wajane wa Wanajeshi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili suala la vijana. Serikali ya Awamu ya Tano ni Serikali ya ‘Hapa Kazi Tu’. Tumeona kuna ongezeko kubwa sana la vijana, ukianza na vijana ambao wanamaliza vyuo hawapati ajira kuna vijana wa kati, hawa vijana wengine wa mitaani ambao wanaishia form four, wanamaliza darasa la saba hawana ajira, hata wale ambao wanajiajiri wenyewe, basi bado Serikali hawajatazama kundi hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka kwenye kundi hilo kuna kundi la wanawake sasa hivi linaongezeka kwa kasi, linakuja kwa speed, waangalie ni namna gani sasa hawa wanawake hawana kazi, hawana vyanzo vya miradi, maendeleo madogo madogo ya kujiendeleza kwa kujikimu na walisema watatoa kila kijiji milioni 50, zile milioni 50 kwa kila kijiji zimekwenda wapi? Hakuna!

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija huku kwenye Halmashauri, vyanzo vya mapato pia wamechukua kupeleka Mfuko Mkuu. Sasa waangalie namna gani vijana wanaingia kwenye mambo yasiyokuwa na maana, akinamama nao wanaingia kwenye janga la mambo ya kujiuza huko, hakuna maana, matokeo yake mnasema tupime UKIMWI, huu UKIMWI utaendelea na utazidi kuendelea kwa sababu sasa kipato hakuna, mtu anatafuta namna ya kujikimu hakuna, Serikali hawaangalii haya makundi ya wapiga kura, vijana, akinamama, wazee, hawawaangalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Mpango sasa tuangalie huu mpango wa mwaka huu unatekelezeka? Tukiangalia huku nyuma yale aliyosema watapeleka milioni 50 kwa kila kijiji hakuna, watawezesha vijana hakuna, watawezesha akinamama hakuna. Sasa nimesoma Gazeti la Nipashe leo Mheshimiwa Rais amesema kuna mikopo ambayo inatoka, kwa kweli kama hii mikopo ipo basi itoke kwa wakati muafaka ili angalau wananchi wapate ahueni, hasa hili kundi ambalo nimelitaja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Zanzibar. Zanzibar ni nchi na imeshasoma bajeti yake, lakini Mheshimiwa Dkt. Mpango na Mheshimiwa Naibu Waziri ni lazima kuna masuala wananchi wa Zanzibar nao wanataka wayapate, wapate ufumbuzi wa mambo haya kwa sababu haya mambo yanakuwa yanaenda hayapati muafaka. Nimwombe Mheshimiwa Waziri atoe kama ni kwenye Gazeti la Serikali au kuwe na kipindi maalum cha kufahamisha wananchi kuhusu hii Akaunti ya Pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Akaunti ya Pamoja imekuwa ikilalamikiwa kwa muda mrefu kwa sababu kule Zanzibar wanasema, sisi tunachangia kiasi gani na Muungano nao huku Tanzania Bara wanachangia kiasi gani, hawajui. Kwa sababu nao kule kuna percent ambazo zinatoka kwenye mambo ya ushuru ziende kule, kuna pesa zinazotoka kwenye Akaunti ya Pamoja ziende kule ili zichochee miradi ya maendeleo, zichochee mambo ya barabara na mambo mengine. Sasa kunakuwa na kizungumkuti, wanasema pesa haziendi kwa wakati muafaka, kinachochangiwa kwa pande hizi mbili hakijulikani, kwa hiyo naomba hili somo walitoe na waangalie ni namna gani ya kufahamisha hawa wananchi wapate kujua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mambo ya ushuru. Bandari ndiyo kitega uchumi cha Tanzania, lakini sasa hivi kwa ukiritimba wa TRA mizigo ya bandari imeshahamishwa, imehamia kwenye bandari za wenzetu. Tunusuru, kuna watu wanatumia mwavuli wa Rais, kumsingizia Rais Mheshimia Dkt. Magufuli kwamba yeye ndiye anawatuma kwenye mambo ya kukusanya kodi, lakini wengine wanaenda kwa utashi wao kwa kutumia mwavuli wa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba wale waende kwa mujibu wa sheria na kile ambacho kinatakiwa wakidai kwa wakati muafaka, siyo kwenda kubambikiza wananchi kodi

kwa kutumia mwavuli wa Rais. Taaluma zao wazitumie kwa sheria na kanuni na siyo kusema Rais kasema, maagizo yametoka juu, hakuna maagizo yaliyotoka juu, wao wana taaluma zao za kukusanya ushuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara hawa wadogowadogo wanalalamika. Hebu wapite huko Kariakoo, watu wanafungua maduka kwa kuvizia, leo Zanzibar waweke pia ni kitu gani ambacho kinatakiwa kikishalipiwa ushuru kwa Zanzibar, Tanzania Bara kisilipiwe ushuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tukiangalia mizigo bandari imepungua, watu wanatafuta njia tu, hata mtu anakwenda South Africa, anakwenda wapi, lakini ilimradi mzigo wake anahakikisha haujapita Bandari ya Tanzania, sasa mapato tutayapata wapi? Serikali itapata wapi pesa kama hawajaboresha utaratibu mzuri wa kukusanya mapato ya Serikali na kuwashirikisha wafanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna nchi iliyoendelea bila wafanyabiashara, hakuna nchi iliyoendelea bila matajiri. Kwa hiyo waangalie, waweke urafiki wa kukusanya kodi na hawa matajiri wasiwe maadui wao, wawe marafiki zao kwa sababu tukiweka mfumo mzuri kwa wafanyabiashara na Serikali nayo itapata Pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili tatizo la vijana wanaomaliza vyuo nimerudia tena mara ya pili, ajira hizi mpya zitatoka mwaka gani, wakija hapa waseme kabisa ajira katika sekta hii zitakuwa hivi na katika zile pande za Muungano hizi ajira zitatoka hivi na zile pande za Muungano ambazo pia zinakaimiwa ajira zake zitakuwa lini kamili na zile Taasisi za Muungano nazo ambazo zinadaiwa wachanganue tusije tukaonekana kama Zanzibar labda hawalipi umeme, Zanzibar hawalipi nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sekta za Muungano wanatakiwa waje wazichambue. Hii Taasisi inadaiwa inatakiwa ilipe, hii Taasisi ni Taasisi hii ilitakiwa itoe percent hii iingize Serikali haijalipa, kwa sababu sijui kama mwananchi wa kawaida kwa uhakika hakuna mwananchi wa kawaida Zanzibar ambaye anadaiwa kuhusu hata hili suala la ... (Makofi)