Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii nami niweze kuchangia hoja iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi niungane na Waheshimiwa Wabunge wote waliompongeza Mheshimiwa Rais kwa wazo hili, lakini naungana na Waheshimiwa Wabunge wote waliompongeza Mheshimiwa Rais kwa maamuzi magumu aliyoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke Rais huyu ana muda wa miaka miwili na nusu au mitatu, hajatimiza mitatu kamili, lakini amefanya mambo makubwa sana ikiwepo kuamua maamuzi magumu ya kufanya Mji wa Dodoma uwe Makao Makuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mimi mwanzo nilipata shock alivyoamua kipindi kile mwanzo tu anaanza. Kwa sababu wakati anaamua ndiyo alikuwa ameamua elimu bure, ndiyo alikuwa ameamua kujenga reli, kununua ndege, kujenga flyover, ndiyo alikuwa mambo chungu mzima katika nchi hii. Nikasema jamani yatawezekana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mshangao mkubwa, leo hii Mji Mkuu wa Dodoma unaendelea kwa kasi kubwa sana, mambo yote mengine ya reli yanaendelea, ndege zimeendelea kuja na karibu zitafika saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naunga mkono hoja hii aliyoitoa Mheshimiwa Simbachawene.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naitakia Serikali yangu kila la heri pamoja na Mheshimiwa Rais ili waweze kutimiza jambo hili na wale wote waliyokuwa wanaona kwamba haiwezekani, basi waje waone aibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti juzi tu wametekeleza kugawa tablets kwa shule zote za msingi jambo ambalo huwezi kuliamini kwa haraka haraka ukizingatia Rais huyu ana muda wa miaka miwili na nusu tu. Amegawa tablets ili walimu wetu wa shule za msingi wazidi kufundisa vizuri. Angalau Mheshimiwa kaka yangu Sugu alisema ile ni ahadi hewa, lakini nimpe taarifa tu kwamba Mheshimiwa Rais ameshaitekeleza, sasa hivi walimu wa shule za msingi wanatumia tablets. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais, naendelea kumwombea kila la heri ili aweze kufanya yale yote aliyokuwa ameyakusudia na tutaendelea kumuunga mkono na kumtia moyo pale panapostahili. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa fursa hii.