Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na nichukue nafasi hii kuunga mkono azimio ambalo lipo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni tangu mwaka 1973 Mji huu wa Dodoma ulishapangwa kuwa Makao Makuu. Umechukua muda mrefu sana takribani maisha ya mtu mzima Serikali ya Tanzania kuhamia katika Mji wa Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kwa maamuzi haya ya haraka na mazito aliyoyachukua kuhakikisha kwamba Serikali sasa inahamia Dodoma. Naamini Marais waliomtangulia awamu ya kwanza, ya pili, ya tatu, ya nne walifanya kazi kubwa ya maandalizi, naye amekuja kuhitimisha lile lililokuwa hamu ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ramani au master plan iliyojenga Abuja Nigeria, ilikuwa master plan ya Mji wa Dodoma. Ukienda Abuja, unaiona Dodoma ambavyo ingekuwa katika miaka hiyo. Nampongeza Mheshimiwa Rais kwamba amewachukuwa wataalam wengi wa ardhi, amewapeleka maeneo mbalimbali kuhakikisha kwamba Mji wa Dodoma unakuwa tofauti na mikoa mingine kwa sababu ni Mji Mkuu uliosubiriwa kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza tena Mheshimiwa Rais kwamba ametoa fedha kwa ajili ujenzi wa stand ya mabasi ya kisasa ambayo litajengwa katika eneo la Nane Nane.

Pia tunajenga uwanja wa michezo wa kisasa ambao utajengwa hapa Dodoma na utachukua takribani watu zaidi ya 100,000. Pia tuna soko la kisasa ambalo halijawahi kujengwa Tanzania katika Mkoa wowote, ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi na ameomba msaada kutoka kwa watu wa Morocco kwa ajili ya ujenzi wa uwanja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sasa Muswada wa Sheria uje kwa ajili ya kuutambua sasa Mji wa Dodoma kuwa Makao Makuu ya Serikali. Naiomba sasa Serikali ifanye haraka kuleta huo Muswada ili sasa Dodoma hata atakapokuja Rais mwingine asiyependa Mkoa wa Dodoma au Mji wa Dodoma, basi asipate nafasi ya kuhamisha Makao Makuu kupeleka Mkoa mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza sana hili azimio na ninaunga mkono azimio hili lililoko mbele yetu.