Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Uamuzi wake wa Kuendeleza Mji wa Dodoma na Kuupa Hadhi ya Jiji

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono azimio hii kwa asilimia mia moja. Mji wetu wa Dodoma umekuwa ni mji wa siku nyingi na Baba wa Taifa alipotamka kwamba Makao Makuu yahamie Dodoma tangu mwaka 1973 ni miaka mingi mpaka sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Magufuli kwa juhudi zake kuhakikisha kwamba sasa anatekeleza lile agizo au wazo la Mheshimiwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwamba sasa Dodoma iwe Makao Makuu. Dodoma ni Jiji kubwa, Dodoma makazi yake yamejengwa vizuri, hakuna squatters, tumefuata master plan, watu wameongezeka, kwa hiyo, kwa kweIi kuna haja ya kupata Jiji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunavyopata Jiji la Dodoma, hata sisi kwenye Wilaya zetu lazima kuna mambo mengi yataboreka kuhusu barabara, huduma za shule, huduma za maji na huduma za afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naunga mkono azimio hili alilosema mdogo wangu Mheshimiwa Simbachawene kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.