Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, fedha za CDG, maombi haya tuliyaleta baada ya Serikali kutuandikia kuwa tutambue na kubainisha miradi viporo ambayo Halmashauri na wananchi waliibua na baadhi ya miradi wananchi wamejikongoja zaidi ya miaka kumi. Tulipopokea barua hiyo tuliona ni ukombozi mkubwa. Mfano sisi Mafinga tulipanga kukamilisha Kituo cha Afya cha Bumilyinga (shilingi milioni 413); kukamilisha Zahanati tatu za Kitelewaji, Kisada na Ulole na nyumba tatu za wauguzi (shilingi milioni 203); kukamilisha hostel katika shule ya sekondari ya Kata Mnyigumba katika Kata ya Rungemba (shilingi milioni 19) na ukarabati wa shule ya msingi Kikombo kujenga madarasa nane (shilingi milioni 179) na jumla shilingi milioni 859. Naomba sana Hazina watusaidie fedha hizi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu gaming/sports betting, kuna dhana kuwa watoto wanaharibika kwa ku-bet,, sio hoja ya msingi, hili ni suala la maadili, tujiulize mbona watu na Taifa tunategemea kodi kwenye vileo? Sports betting imeshakuwa kwa kasi sana, kwa mwaka 2017 iliingiza shilingi bilioni 28.2 ambayo ni sawa na bajeti ya Wizara ya Habari.

Mheshimiwa Spika, kuna potential kubwa sana kwenye sports betting, kitu muhimu ni usimamizi bora na kuweka mazingira bora ya kuvutia wachezaji wengi, kwa sababu kinyume chake watu wanakimbilia kucheza online nje ya nchi. Hivyo basi ushauri wangu:-

Mheshimiwa Spika,tulipoanza ili kuvutia wawekezaji tuliweka kodi asilimia sita ya GGR, hivi sasa kwa kuwa industry imekua, tuongeze kutoka asilimia sita hadi asilimia 20 ya GGR. Lakini wakati huo huo tuvutie zaidi wachezaji wawe wengi ili tufanikiwe.

Mheshimiwa Spika, tupunguze kodi kwa mshindi kutoka asilimia 18 ambayo ni VAT tuifanye asilimia kumi as a capital gain. Kwa kufanya hivyo itavutia wachezaji wengi na Serikali itapata zaidi kutoka asilimia sita hadi asilimia 20 ya GGR. Mfano mchezeshaji akikusanya shilingi milioni 100 maana yake Serikali itapata shilingi milioni 20 kama asilimia 20 badala ya shilingi milioni sita ya sasa ambayo ni asilimia sita.

Sasa katika hiyo shilingi milioni 100 ikiwa jumla ya washindi wakawa wamepata shilingi milioni 15 maana yake asilimia 18 ni shilingi milioni 2.7 ukijumlisha na ile shilingi milioni sita ya asilimia sita jumla Serikali itapata shilingi milioni 8.7, lakini ingekuwa ni GGR ya asilimia 20 Serikali ingepata shilingi milioni 20 na pia ingepata asilimia kumi ya shilingi milioni 15 as capital gain ya shilingi milioni 1.5 hivyo jumla Serikali ingepata shilingi milioni 21.5 badala ya shilingi milioni 8.7. Huu ni mfano mdogo tu lakini ambao unaihakikishia Serikali mapato kutoka kwenye GGR.

Mheshimiwa Spika, hali ilivyo sasa watu wengi wana- opt kucheza online kwenye makampuni ya nje na Serikali inakosa fedha. Sio dhambi kabisa kuvutia wachezaji wengi hasa kwenye sports betting. Mfano Australia kati ya watu kumi, watu saba wanacheza sports betting, so tuvutie wachezaji wengi tupate GGR. Ahsante