Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa ni migogoro ya muda mrefu hapa nchini. Serikali haijaonesha mikakati ya dhati ya kumaliza migogoro hii. Mara nyingi Wabunge wameitaka Serikali imalize migogoro hii iliyodumu kwa muda mrefu, kuwepo na mipango sahihi ya ardhi, hakika kutapunguza migogoro hii. Naishauri Serikali kwa kushirikiana na Wizara mbalimbali pamoja na Halmashauri za Wilaya ziweke bajeti inayotosheleza na inayotekelezeka ili zoezi la upangaji wa matumizi bora ya ardhi liweze kufanyika au kutekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pembejeo za kilimo na mbolea; kumekuwa na tatizo la ucheleweshaji wa mbolea kwa wakulima hasa msimu unapoanza. Ucheleweshaji ni jambo moja ila hata mbolea halisi inayohitajika na wakulima kulingana na ardhi zao ni tatizo lingine. Tatizo hili ni kubwa sana na linaleta athari kubwa kwa wakulima.
Kwa kuwa Viwanda vya Mbolea ni vichache na kwa kuwa kilimo ni jambo endelevu na hitaji katika maisha ya kila siku ya wananchi wetu, nashauri Serikali iwe na mpango wa muda mrefu wa kuwa na viwanda vya mbolea ambavyo vitaendeshwa na Serikali ili kuondoa na kupunguza kabisa urasimu na upatikanaji wa mbolea hapa nchini.