Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, na mimi naomba niungane na wenzangu kwa kuipongeza Wizara ya Fedha, inafanya kazi vizuri hasa kwenye mambo ya forex stabilization pamoja na inflation, wamefanya vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, vilevile naiomba Serikali irudishe haraka Tume ya Mipango inayoonekana. Inawezekana tuna shughuli za mipango lakini tungeiona Tume ya Mipango ambayo ni huru. Wakati kama huu wa leo ambapo tuna miradi mikubwa mingi ya muda mrefu, inahitaji vyombo mbalimbali kwa ajili ya kusimamia hiyo miradi. Nina imani kuwa Tume ya Mipango ingesaidia sana kuingalia; je, mradi wetu wa standard gauge utakwendaje? Hela kwa ajili ya standard gauge itatoka wapi? Kwa vile hii ni investment ya muda mrefu, itahitaji vilevile na financing ya muda mrefu na vilevile miradi kama ile ya Stiglers Gorge. Kwa hiyo, ni muhimu sana Serikali ikaliangalia hili, ikalirudisha na hii Tume ya Mipango iwe huru. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni suala zima la namna gani tunaweza kuongeza mapato ya Serikali hasa yale ambayo yasiyokuwa ya kodi. Nina imani kuwa Msajili wa Hazina (Treasury Registrar) ni muhimu sana kutuletea mapato yasiyokuwa ya kodi. Hii italeta unafuu kwa walipa kodi. Tutaonekana Tanzania tunapunguza hata viwango vya kodi. Kodi zimekuwa nyingi mno ambazo hazihitajiki. Investment za TR ni shilingi trilioni 47. Asilimia kumi tu ni shilingi trilioni 4.7, ni hela nyingi kama Serikali tukiitumia vizuri hii ofisi. Ukiangalia bajeti yao ilikuwa kuileta Serikalini shilingi bilioni 500 tu, ni hela kidogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Waziri wa Fedha na hasa TR ayape malengo haya mashirika. Tumeona mashirika kama NMB ilikuwa imefilisika, lakini leo kwa ajili ya utendaji mzuri wa management inailetea Serikali dividend kubwa, CRDB inafanya vizuri, nina imani nayo tumepata dividend kutoka CRDB. Kwa hiyo, hilo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, lingine ni ulipaji wa madeni. walimu hawajalipwa stahiki zao. Jimboni kwangu kuna walimu karibu 1,000 wanadai toka mwaka 2017 shilingi milioni 482. Tunashindwa nini kuwalipa walimu? Wako frustrated, muda mwingi wanakuja kufuatilia hela zao Dodoma. Sasa unaangalia, hela anayofuatilia Dodoma ni kidogo sana.

Mheshimiwa Spika, je, nauli tu ya kwenda na kurudi watajikuta ya kwamba hata hiyo shilingi milioni 482, nayo imepotelea kwenye nauli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho, ushauri wangu kwa shilingi milioni 50, hizi ni mfuko wa kuzunguka. Mfuko wa kuzunguka maana yake siyo matumizi. Tumeona jana Mheshimiwa Rais amefanya uamuzi mzuri sana wa kushauri tuimarishe Benki ya Wakulima. Ni kwa nini tusiitumie Benki ya Wakulima ikapewa hizi pesa? Siyo lazima iwe mtaji, wawekewe tu hizo shilingi milioni 50 kwa vijiji vyetu, hasa kwa kuanzia ili wao wasimamie, kwa sababu tuna imani Benki ndiyo wataalam wa kukopesha na wataalam wa kutumi vizuri mifuko kama hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ushauri wangu kwa Wizara ya Fedha na kwa kweli ipo kwenye Ilani, tukishindwa hili, hata kuitengea Benki ya Wakulima ikawasaidie wakulima huko vijijini, shilingi milioni 50 kwa kila kijiji ili vijana wafanye ufugaji...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.