Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa busara ya meza yako, na mimi nimepata fursa ya kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, ni bayana kabisa kwamba budget performance ya nchi hii inaendelea kuporomoka siku hadi siku. Haya huhitaji kutumia microscope kutafuta details. Ukipita vijijini unakutana na watoto ambao bado wanaugua utapiamlo. Bado suala la lishe tu ya Watanzania halijaweza kukidhi angalau tukawa na Watanzania wenye afya bora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mambo ambayo ukiyatazama kwa undani unagundua kabisa kwamba performance yetu bado ni chini sana. Suala la makusanyo ya mapato kupitia TRA kila siku tunaambiwa makusanyo yanapaa kwa kasi ya ajabu, wakati biashara zinakufa. Hivi uhusiano huo uko wapi? Hayo mapato wanayokusanya, yanatokana na nini? Wamegeuka wanyang’anyi sasa TRA, wakikuta unajikakamua, unakazana na kabiashara kako, kila siku wanatamani kuingiza aina mpya ya mfumo wa kukubabaisha na kukusumbua na kukubambika ili mwisho wa siku wapate ile fahari wanayoitafuta ya kusema mapato ya nchi yanakua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, alama nyingine ni upelekaji wa fedha za maendeleo/fedha za miradi. Mmeona katika Wizara nyingi sana zilizowasilishwa hapa na wakati tunafanya shughuli za Kamati, taasisi na Idara nyingi sana za Serikali fedha za maendeleo zimepata asilimia sifuri mpaka asilimia tano. Hicho ni kigezo cha kusema hatu-perform kama Serikali. Waheshimiwa Wabunge wa CCM wametupa ushahidi mzuri tu kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi haina mipango, ndiyo maana tunaendesha nchi kwa mfumo wa butua butua, yaani linalozuka mezani siku hiyo, ndiyo linalozungumzwa ndiyo linalofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la msingi sana ambalo tukilijadili kwa details unaweza kushangaa. Kuna miradi kama Bwawa la Kidunda. Kwa taarifa nilizopewa kwa waliokuwepo bwawa hili lipo kwenye Bajeti za Serikali tangu mwaka 1974, lakini mpaka leo bwawa hilo halijawahi kujengwa na bado linaitwa mradi wa kimkakati.

Mheshimiwa Spika, hivi hili neno mkakati Serikali ya CCM mna tafsiri yake sahihi ama huwa mnalizungumza tu? Ukilifanyia tathmini hilo bwawa matokeo yake ambayo yangeipa nchi hii ni makubwa sana, umeme, umwagiliaji, miradi ya kilimo na kadhalika. Linaitwa mkakati, linatengewa fedha hewa, haziendi bado linaitwa mkakati na mwaka huu nimeliona lipo mkakati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la performance ya Bunge, hili niombe tulitazame tena. Unajua siku hizi tunakimbizana sana humu ndani ya Bunge. Dakika za kuchangia tano, muda wa kukaa masaa mawili, tarehe za kuingia pungufu. Hivi hili suala tutakwendaje nalo mbele kwa utaratibu huu? (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napokea taarifa ya Mheshimiwa Waziri lakini nimeeleza, unaitwa mradi wa kimkakati tangu mwaka 1974. Je, tafsiri ya neno kimkakati tunaifahamu? Hiyo ndiyo hoja ya msingi. Ahsante.