Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Dakika tano sijui kama nitazitumia vizuri, ngoja nianze. Nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu na Makatibu Wakuu na wasaidizi wake wote.

Mheshimiwa Spika, kwanza nianzie kwenye suala la pesa/dola. Naipongeza Wizara ya Fedha tuliongelea suala la dola huko nyuma, wamefanya marekebisho kwamba ukienda ku-change dola sasa utaombwa passport utapewa risiti. Naomba kushauri, hamjafanya kazi vizuri kwa sababu ukienda ku-change dola bila kuomba EFD machine, hawakupi. Sasa hiyo control mnaifanyaje? Lengo ni zuri lakini bado yako maduka yanauza dola bila kutaka kitambulisho, Hawa wakoje na mnawaonaje na mnawaangalia vipi?

Mheshimiwa Spika, la pili kwa haraka, niongelee madeni ya ndani. Nawapongeza juzi kwenye Kamati mmeniambia mmeshalipa madeni ya ndani shilingi 1.1 trillion.

Tatizo langu ninalolipata, kule mikoani kuna ndugu zetu ambao wanafanya biashara na Serikali, wanadai shilingi milioni tano, shilingi milioni 10 au 20 na inaonekana Wizara ya Fedha mnapeleka madeni yale kwa kutaja jina alipwe Bulembo. Sasa kuna watu wanaendelea kulipwa, kuna watu wana hela ndogo hawajawahi kulipwa. Naomba mliangalie upya. Kwenye madeni ya mwaka huu mnayoyalipa, uhakiki ni mzuri, lakini hela inapotoka asiwe ana-appear mtu mmoja katika mkoa fulani ndiyo analipwa na wale wengine nao wapewe haki ya kulipwa madeni hayo.

Mheshimiwa Spika, lingine ni ukusanyaji wa kodi kwa njia ya elektroniki. Nataka kuuliza swali, kila Wizara ina mtandao, je, mmeshaunda chombo cha kwenda kuhakiki ile electronic kwenye maeneo mengine? Maana sehemu moja iki-collapse, kama juzi ilivyotokea kwenye EFD katika nchi hii, watu wote walipata shida.

Je, mmeshaweka chombo kingine pembeni, kikishindikana hiki mbadala ni huu? Ni vizuri kwa sababu watu wameshaamua kulipa kodi, lakini system inapoharibika tunapata hasara kubwa na haiwezi kurekebika.

Mheshimiwa Spika, suala la tatu, ni bahati nasibu ya Taifa. Napingana na watu waliokuwa wanasema sijui Biko sijui nani, hapana. Mwisho tutafika mahali tutasema viwanda visitengeneze bia. Nchi zilizoendelea, Bahati Nasibu ni eneo linalokusanya pesa nyingi katika nchi. Ni chanzo kizuri, lakini huko nyuma Bahati Nasibu ya Taifa tulikuwa tunapata asilimia 10 kwenye michezo. Sisi wanamichezo kwenye timu za Taifa, timu gani ilikuwa inapata kule.

Mheshimiwa Spika, naiomba Wizara ya Fedha muimarishe suala hili eneo hilo, kwamba Bahati Nasibu ya Taifa iende mpaka vijijini, tukusanye hela. Ni hela za hiari kama kunywa pombe, kama kunywa chai, kama kunywa soda. Wale waliokuwa wanapinga watoto wanaumiza hela, haya. Mnawapa hela vibaya, matumizi ndiyo haya mabaya, lakini hatuwezi kuondoa Bahati Nasibu ya Taifa kwa sababu ni chanzo cha mapato katika Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, lingine ni elimu kwenye utakatishaji wa pesa. Hivi lini mnaenda kutoa elimu kwa hawa watu wanaotakatisha? Kuna jambo linafanyika sasa ambalo najua hamjalifanya. Mimi kusema ndiyo kazi yangu. Suala la kwamba kuna watu wanaenda kupata pesa Ulaya, wanalipwa huko, wanakusanya dhahabu hapa nchini, kwa sababu hamdhibiti dhahabu, wanaenda kupeleka kule hela na hela zile zinakuja kwa njia nyingine. Kwa nini ninyi mnaangalia mabenki tu? Huku pembeni mbona hamuangalii na bado mchezo huu wa hela chafu upo? Nilikuwa naomba Wizara ijielekeze huko zaidi.

Mhesimiwa Spika, la tano, kodi ya mabango; mwaka 2017 tuliwaambia kwenye kodi mlizotoa Halmashauri kwenda kwenye mabango. Mwaka huu imekusanywa kama asilimia 52, hamtaki ushauri. Njooni tuwape elimu wenye uzoefu wa shughuli hii, kwanini mnakuwa wachoyo? Style ya kukusanya kodi hii ipo, inaonekana kwenye Halmashauri walikuwa wanakusanya vizuri kuliko ninyi. Ninyi mmempelekea TRA, anafanya kama kazi ya ziada. Kwa hiyo, Halmashauri inaonekana ilikuwa inakusanya vizuri, ninyi Wizara hamkusanyi vizuri.

Mheshimiwa Spika, la mwisho ni Bodi za Mashirika; Bodi za Mashirika hizi, watu wanateuliwa, wanaambiwa walipwe hela miezi mitatu. Wakishapata ile hela, siku wakiitisha kikao, walikuwa watu kumi wanaenda wanne, kwa sababu siku anaenda halipwi, anaenda kula korosho na maji, itakuwaje? Kwa nini msiangalie? Ufanisi unapungua. Kwa nini tuone kama hizi bodi zinafaidika zaidi? Zilikuwa zinasimamia mambo mengi, lakini nini kinamshawishi mtu kwenda kwenye kikao kile hata kama umemteua?

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo hili naona mwende upya mwangalie zaidi. Siyo kuwaondolea watu hicho kidogo mlichokuwa mnawapa, si ni haki yao? Si wanasimamia zile taasisi za mabilioni? Mtu unamlipa shilingi 500,000 unasema inaishia hapo. Eneo hili naomba mwangalie zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho, nawapongeza tena Wizara, chapeni kazi, changamoto mnazozipata, ndiyo maana mlipata nafasi hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja.