Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mujibu wa kanuni ina jukumu na kwa mujibu wa sheria tulizonazo inajukumu la kuleta mbele ya meza yako sheria ndogo zote ambazo zimekwisha kutangawa kwenye Gazeti la Serikali na inawekwa mbele ya meza yako tukufu na baada ya Kamati ndogo Kamati ya Sheria Ndogo kumaliza kazi yake hii yote nzuri kama ilivyofanywa leo. Ofisi ya Waziri Mkuu inajukumu la kupokea maoni yaliyotolewa na Kamati ndogo na ndiyo maana Waheshimiwa Wabunge wawe watulivu wajue tunachotaka kusema. Na wakati mwingine utaratibu wa kelele kelele siyo wa Kibunge.
Mheshimiwa
Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu ina jukumu la kupokea maoni na mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Sheria Ndogo na kuyawasilisha kwa Wizara zote husika kwa jinsi yalivyochambuliwa na Kamati ya Sheria Ndogo. Hata Mheshimiwa Halima anajua, nimekuwa nikienda mpaka kwenye Kamati kupokea majedwali hayo kwa niaba ya Wizara zote.

Ninasimama hapa kusema yafuatayo, kwanza ninampongeza Mwenyekiti kwa kazi yake nzuri; pili, ninawapongeza Wajumbe kwa kazi yao nzuri; na tatu ninatambua yale yaliyojiri kwenye taarifa ya Kamati ndogo na yamewekwa vizuri sana na summary ya Mheshimiwa Mwenyekiti wakati akihitimisha hoja yake. Ni yapi? (Makofi)

Kwa mujibu wa sehemu ya tatu ya Kamati za Kisekta Mtambuka ambayo kifungu kidogo cha (c) kinaitambua Kamati yetu ya sheria na kifungu cha 11 kimeelezwa vizuri na Mwenyekiti wakati akihitimisha hoja yake, wajibu wa Kamati Ndogo wameutekeleza Kamati inayoshughulikia Sheria Ndogo wametekeleza vizuri mambo makubwa yaliyojiri ambayo ninatokanayo na nitayawasilisha kwenye Wizara husika kama yalivyowekwa mezani na Mwenyekiti wa Kamati Sheria Ndogo ni pamoja na hayo mawili aliyoyazungumza kuhusu majedwali yanayoenda na sheria mama. Lakini vilevile makosa madogo madogo ambayo yamekuwa yakijitokeza na kujirudia katika sheria ndogo zina zotungwa yanayoendana kinyume na sheria mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo limejitokeza suala la Watendaji wetu wanaosimamia ama wanaoshughulikia sheria hizi ndogo kutokuwa na umakini katika kufanya kazi yao. Jambo hilo ninaomba nilichukue pia na liweze kufanyiwa kazi ya kutosha na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile amesema ziko Wizara ambazo zimejitokeza kwa nguvu kidogo kwenye taarifa ambazo zimekuwa zikichambuliwa na Kamati yetu Kamati ya sheria ndogo, nazo tutazifikishia majedwali hayo ili yaweze kufanyiwa kazi sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulihakikishia Bunge lako tukufu kadri tunavyofanya kazi na Kamati ya Sheria Ndogo tumekuwa na mabadiliko makubwa na tunaishukuru sana Kamati ya Sheria Ndogo imekuwa ni msaada mkubwa sana kwa uandishi wa sheria ndogo ndani ya Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawashukuru sana Wajumbe wa Kamati ya Sheria Ndogo na sisi kama Serikali tutaendelea kufanya nao kazi kwa karibu ni kwa maslahi ya Taifa na nchi yetu na si kwa maslahi ya mtu mwingine yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa niaba ya Serikali tutayatekeleza hayo yote.