Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Dr. Adelardus Lubango Kilangi

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, kwanza nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Chenge Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kwa mawasilisho yake na kwa hoja alizotoa na wote tunamfahamu nakumkiri Mheshimiwa Chenge katika umahiri wake wa sheria. Kwa mimi binafsi nimtangulizi wangu, ni kaka yangu amekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwa hiyo, huwa napata pia mawazo na ushauri mwingi kutoka kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika masuala la sheria siku zote kuna mambo mawili makuu ambayo hata Mheshimiwa Chenge anayafahamu vizuri sana. Kuna masuala ya misingi yaani principles na kuna masuala ya utaratibu yaani procedure au enabling procedures. Tunapokuja suala la udhibiti wa Bunge katika suala la utungaji wa Sheria Ndogo na tukaja kwenye principles hakuna ubishani, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ile Ibara ya 97(5) imeeleza vizuri. Hata hii Interpretation of Laws Act nadhani ni kifungu cha nne haina ubishi. Lakini pia misingi hii kwa wanasheria wanajua iko kwenye principles za Administrative Law, sijui kwa Kiswahili tunaweza kusema Sheria ya Utawala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika principles hakuna shida na tunakubaliana Serikali na Kamati na kila mtu. Kuna changamoto kunapokuja kwenye utaratibu na ndiyo maana Mheshimiwa Chenge mwenyewe katika taarifa hii na ameirudia wakati anahitimisha kwamba waliona na ninapenda tena kurudia kusoma hii sehemu ukurasa wa nne wa ripoti hii kwamba; hata hivyo udhibiti huo yaani udhibiti wa Bunge katika utungaji wa sheria ndogo siyo wa moja kwa moja kwa sababu Bunge halina mamlaka ya kuingilia mchakato wa kutungwa kwa sheria ndogo yoyote mpaka sheria ndogo inapotangazwa katika Gazeti la Serikali na kuwasilishwa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ametueleza vizuri sana Mheshimiwa Chenge vizuri ametuelimisha taratibu zinazotumika katika Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Lakini kwa nini sentensi hii iliwekwa ni kwa sababu ya ile concept hii ni delegated legislation. Kwa hiyo, Bunge kimsingi haiwezi tena likaja na kuanza kujadili zile sheria ndogo kwa sababu litakuwa limefuta ile concept ya delegated legislation na ndio hiyo changamoto pekee iliyopo na ndiyo maana akaeleza juu ya taratibu hizi mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nilitaka niseme, hata ukienda kwenye kanuni zetu za Bunge Toleo sasa la Januari 2016 ukiangalia ile Kanuni 80 mpaka ya 93 zinahusu utungaji wa sheria unaofanywa na Bunge, hakuna kanuni inayozungumzia Bunge litakavyofanya kazi dhidi ya sheria ndogo ambazo zimeshatungwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tungekuwa tunatumia huu mfumo wa kwanza aliutaja wa affirmative resolution procedure tungekuwa na kanuni hizo kwenye Bunge letu zitatuongoza tunapotunga sheria tunazoziita kubwa huu ni utaratibu, tukija tunaposhughulika na sheria ndogo huo ni utaratibu hatuna huo utaratibu ni kwa sababu tunatumia ile aina ya pili aliyoizungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niseme na nikumbushe na Mheshimiwa Chenge ni mahiri sana katika hili; katika mfumo sasa wa Common Law siyo wa Commonwealth Parliament, wa Common Law sheria ndogo ndogo kama zina matatizo nini utaratibu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu siku zote umekuwa kupitia kitu kinaitwa judicial review na hiyo inafanyika judicial review moja wapo ya misingi ya judicial review ni kama ile sheria iko ultra vires yaani inapingana au imejipa ukuu zaidi ya ile sheria mama ambacho Mwenyekiti alikuwa anakieleza hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, upo utaratibu katika mfumo wa sheria wa Common Law. Sasa nilitaka tu ku-share hilo na kuonyesha shida kidogo. Naomba dadika moja kuna kitu cha muhimu nimalizie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa yamezungumzwa mapungufu katika uandishi wa sheria. Tunayakiri haya kwamba yametokea mapungufu mara kadhaa katika uandishi wa sheria ni mojawapo ya changamoto ambazo Afisa Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekuwa nazo na ndiyo maana mwaka huu Mheshimiwa Rais akaamua kutoa maelekezo ya kuunda.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuusuka upya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kwa hiyo zile changamoto zilizozunguzwa za uandishi za upungufu wa watu na kadhalika, hizo zitashughulikiwa na zinaendelea kushughulikiwa tunavyoongea, naomba kuwasilisha.