Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kwenye Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba wengi wetu sisi Wabunge hapa ndani tuna mikataba na wananchi waliotutuma tuje tuwawakilishe katika Bunge lako tukufu. Ipo mikataba tuliyoingia kuna psychological contracts watu wana matarajio na sisi lakini haya yote yatatimilika pale ambapo siyo tu kwa kupitisha bajeti ya Serikali, lakini ni pamoja na kuangalia masharti hasi yanayotokana na sheria mbovu katika nchi hii ambayo yanaruhusu mianya mikubwa ya upotevu mkubwa wa fedha katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye muktadha wa wasilisho la Sheria Ndogo hasa nikijikita kwenye dhana nzima ya local content policy. Ninaomba nichangie kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikichukulia mfano wa Kampuni ya PUMA ambapo Serikali ina hisa asilimia 50 na wawekezaji wana hisa asilimia 50. PUMA kwa muktadha wa sheria hasi na sheria zenye vigezo vigumu visivyotekelezeka ni dhahiri kwamba PUMA anaenda kupoteza kiasi kikubwa cha mapato yake. Kwa sheria iliyopo ambayo ni sheria hasi, PUMA anapoteza lita 2,500,000 kwa mwezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu tukiangalia nafasi ya PUMA au umuhimu wa PUMA katika ujenzi wa uchumi wa taifa hili; juzi tu hapa nikiwa pamoja na Kamati ya PIC tunaona PUMA alitoa shilingi bilioni tisa gawio la Serikali. Ni dhahiri kwamba hatutasimama katika kuona kwamba sheria hizi zinafanyiwa marekebisho ya haraka ni dhahiri hata hili gawio pengine tunaweza tukalipoteza kwa siku zijazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muktadha wa sheria hii ninaomba nieleze Bunge lako hili tukufu kwamba Shirika la TIPER ambalo Serikali ina asilimia 50. Tukija SINOTASHIP ambao ni Wakala wa Meli Tanzania kupitia ushirika wa Uchina na Tanzania itapoteza kazi kubwa nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, ninapoongelea Benki ya NBC ambayo Serikali ina hisa asilimia 30; lakini ukija NMB ambapo Serikali ina hisa asilimia 31 ni dhahiri Serikali ama nchi kwa ujumla wake tutashindwa ku-realise faida ya kuwa na uwekezaji wa aina hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia hitaji la local content policy inaongea pale siyo tu kwamba kampuni ya kizawa iwe na asilimia 51 ya uwekezaji, lakini pia kuna takwa la kisheria kuhusu rasilimali watu kwamba katika mfumo huu wa local content policy, asilimia 80 ya top management ni lazima wawe wazawa wa Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na Dkt. Mpango ni shahidi juzi nilimuona, lakini siyo hivyo katika mazungumzo yangu na Dkt. Mpango nikimuelezea dira na mwelekeo wa makao makuu ya nchi hapa Dodoma niliweza kumtahadharisha nikamwambia kwamba Mheshimiwa Dkt. Mpango hapa tunapoongea wapo baadhi ya Mabalozi ambao hawajajua hata ofisi wataijenga wapi Dodoma hapa, lakini tayari wameanza ku-grab ardhi na kupita kwenye Halmashauri zetu kutafuta resources za kuweza ku-grab.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hatutakuwa na mpango madhubuti wa kuweza kulinda wazawa wetu katika Taifa hili ili waweze kushiriki kupitia mpango huu wa local content policy kwenye lile takwa la kisheria la asilimia 80 ni dhahiri tutaenda bado kutokuwa na majibu sahihi hasa tunapoongelea ukuaji mkubwa wa ukosefu wa ajira nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuongea na Mheshimiwa Mpango, lakini pia niliongea na Mstahiki Meya na yeye pia alikiri kwamba ni muhimu sana tukawa na sheria nzuri zenye tija ambazo zitaweza kumlinda mzawa wa Taifa hili ili na yeye aweze kushiriki kwenye ujenzi wa uchumi wa Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzangu wote wameongea na kimsingi wote tunaona umuhimu wa Serikali kufanya mapitio ya haraka ya sheria hii. Kama tuliweza kuleta masuala mengi kwa hati ya dharura na hili hata ikibidi liende nje ya utaratibu lije kwa haraka. Hii ni kwa sababu Ofisi ya TR ina malalamiko makubwa, ina mzigo wa mashirika mengi ya Serikali yasiyokuwa na tija katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima na unyenyekevu ninaomba sasa nimalizie kwa kuomba kwamba Serikali kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Wizara husika iweze kutendea haki suala hili ambalo Wabunge wengi wamechangia na kuguswa kwa aina yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.