Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati

MHE. WILFRED M. RWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe ushauri kwa Mheshimiwa Waziri, wataalam na Serikali nzima ya Chama cha Mapinduzi kwamba wanapopanga miradi ya kutekelezwa ni vema wakaanza kuchukua dira tofauti na kuangalia dira ya uchaguzi. Miradi mingi inapangwa kwa ku-focus uchaguzi 2020, 2019 kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, matokeo yake wanakuwa over ambitious, wanapanga miradi ambayo kiukweli haiwezi kutekelezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini nimezunguka katika miradi mbalimbali. Ukimsikiliza Mheshimiwa Waziri humu ndani, lugha anazoongea na wakati akijibu maswali wanazungumzia lugha ya kwamba kila kijiji lazima kiwekewe umeme kwa sera ya REA lakini kwa watu tuliotembea, tuliokwenda kwenye maeneo kukagua miradi unakuta kwenye kijiji ni kitongoji kimoja ndiyo kina umeme na kitongoji chenyewe unakuta ni watu watatu, ni kaya nne au tano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningemuomba Mheshimiwa Waziri, ili kutowaweka Wabunge katika sakata baya sana ifikapo wakati wa uchaguzi, wataulizwa maswali huo umeme uko wapi kwa kila kaya, badala yake ningemshauri hii lugha ya kila kijiji ibadilike na kuwa kwamba mahali ambako kutapitishwa umeme au kwenye centre ya maeneo fulani, ili wananchi tuanze kuchukua sera mpya, wananchi waanze kuwekewa mpango wa kuvuta wao wenyewe umeme kutoka sehemu mnazoweka umeme. Hii lugha ya kila kijiji haipo, haitekelezeki, kutokana na kutolewa mafungu machache hiki kitu hakitekelezeki, ni uwongo uliokubuhu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni suala la ulipaji wa wakandarasi. Naipongeza taarifa ya Kamati ya Bunge imezungumza ukweli kwamba, wakandarasi kwa mfano wa Phase III, tangu mwezi Oktoba mpaka leo watu hawajalipwa pesa. Matokeo yake hawa watu wamesaini mikataba ambayo kimsingi baada ya miaka miwili wanapaswa wawe wamemaliza mikataba hii. Tutaomba Mheshimiwa Waziri atueleze ukweli kutokana na ucheleweshwaji wa hawa wakandarasi Serikali inaingia hasara kiasi gani ili tujue upande wa pili wa shilingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, kuna mdudu huyu ambaye ameingia, mimi namuona kama mdudu. Hili suala linaloitwa uhakiki, malipo mengi ndani ya Serikali yanachelewa kutokana na kuambiwa kuna suala la uhakiki. Hili suala la uhakiki linaanzia REA wanahakiki kivyao, inakuja Wizara inahakiki na Hazina wanahakiki, hivi Serikali gani ambayo hamuaminiani? Kwa nini hamuaminiani? Kwa nini kusiwe na centre moja, kama ni uhakiki ufanyike katika centre moja badala ya centre tatu, matokeo yake miradi inachelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni compensation kwa wananchi. Kwa mfano, katika mradi wa KV 400 wa Singida - Arusha mpaka Namanga, wananchi wamezuiwa kuendeleza maeneo yao kwa sababu pale kutapitishwa mradi, tunajua sheria inazungumzia miezi sita, hawa wananchi sasa hivi ni miaka miwili. Mheshimiwa Waziri tutaomba uwaelezee Wabunge na wananchi wasikie hatima yao ya kulipwa compensation ni nini? Kama miaka imepita, miezi sita imepita, je, watalipwa interest kwa kucheleweshwa au vinginevyo izungumzwe wazi hapa, wananchi waruhusiwe kuendeleza maeneo yao kwa sababu Serikali imeshindwa kufanya compensation na hawajui hatima yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ni umeme katika vijiji mji. Nashukuru huu mradi umeanza uko Kigamboni na unategemewa kutekelezwa. Naomba kujua katika Vijiji vya Ijuganyondo, Buhembe, Kahororo, Kibeta nini hatima yeke katika suala hili. Mnajua sisi wananchi wa Mjini (Bukoba Town) umeme ni deal, hatuulizii stakabadhi ghalani, hatuulizi pembejeo sisi umeme ndiyo mahala pake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.