Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata fursa ya kuchangia kwa maandishi. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote walioandaa hotuba hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu kuwa ofisi za Ubalozi zimepewa jukumu la kutoa Visa kwa wageni mbalimbali wanaotaka kufika nchini kwa shughuli mbalimbali, suala la Visa rejea. Katika utoaji wa Visa rejea kumekuwa na ucheleweshaji sana kuwapata waombaji wanaotoka katika zile nchi ambazo nchi yetu inawapatia Visa hizo. Kuna nyakati Visa rejea hutolewa baada ya miezi mitatu na wakati mwingine waombaji hawapati majibu kabisa. Hii inaleta adha kwa wale wageni wanaotaka kuja pamoja na Maafisa Balozi. Hali ya kuchelewa au kutopata Visa rejea, husababisha Serikali kukosa mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kulipitia upya sharti la Visa rejea ili kwenda na wakati kwa kufungua milango ili wageni waweze kuingia. Mfano watalii, wawekezaji, wafanyabiashara na wageni wengine ambao huja kwa shughuli za mikutano na ziara za utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, malipo ya ada ya Visa kuwa juu na kwa dola. Kuna baadhi ya mawakala wamekuwa wakitoa pesa juu sana kwa ajili ya Visa mfano baadhi ya mawakala wa Saudi Arabia wamekuwa wakitoza ada si chini ya dola 600, sambamba na hilo kuna baadhi ya mawakala hawana ofisi maalum, ni budi Wizara kufanya uhakiki wa mawakala wote ili kuwaondolea adha Watanzania kulanguliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 66 ajira mpya, pamoja na kupata kibali cha kuajiri watumishi 10 bado ofisi nyingi za Ubalozi zina upungufu wa wafanyakazi wanadiplomasia. Hebu Serikali ifanyie kazi ili wapatikane na kutosheleza ili kuleta ufanisi katika utendaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafasi za kazi nje ya nchi. Tanzania imekuwa ikisisitiza umuhimu wa Watanzania wana diaspora waishio nje kuchangia uchumi wa Taifa letu kwa kuleta mapato wapatayo huko ughaibuni. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha jambo hili linaenda sawa na kuleta tija kwa nchi? Mkakati upoje ili Watanzania wote waishio ughaibuni wafahamike wapo nchi zipi na wanafanya kazi au shughuli zipi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata fursa ya kuchangia kwa maandishi na naunga mkono hoja.