Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu pembejeo; kumekuwa na ucheleweshaji mkubwa wa pembejeo kwa wakulima hivyo kuathiri wakulima wetu na kupelekea ufanisi kuwa mdogo katika kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Mfano, Wilaya ya Nachingwea, mbegu na mbolea za ruzuku mpaka sasa zipo maofisini, hazijawafikia wakulima kutokana na kuchelewa. Aidha, kumekuwa na utaratibu mbovu wa kuwatumia wafanyabiashara kusambaza pembejeo. Hali hii inapelekea udanganyifu mkubwa kati ya Wasambazaji na Maafisa Kilimo.
(d) Mfumo huu kutokana na kuchelewa kwa malipo unachangia ununuzi holela wa mazao kwa kutumia vipimo visivyo sahihi „KANGOMBA‟
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri ni kwamba malipo yafanyike kwa wakati ili kuwakomboa wakulima, mabenki yabanwe ili kupunguza riba kwa Vyama vya Msingi. Maafisa Ushirika wawe wanabadilishwa vituo mara kwa mara kwa maana waweze kuwa na vikwazo vikubwa kwa maendeleo ya wakulima kwa kushirikiana na wafanyabiashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya umwagiliaji; miradi mingi ya umwagiliaji haifanyi kazi kutokana na usimamizi mbovu unaofanywa na ofisi za Kanda. Wilayani Nachingwea kuna miradi mikubwa miwili ya umwagiliaji Mitumbati na Matikwe, miradi hii imepewa pesa nyingi lakini haijafikia malengo ya kutoa huduma kwa walengwa kutokana na ubadhirifu na kukosekana kwa usimamizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri ni kwamba, usimamizi wa miradi hii usisimamiwe na ofisi za Kanda, badala yake pesa zielekezwe Halmashauri na zitasimamiwa na Wataalam wetu na Madiwani. Elimu ya mara kwa mara itolewe kwa wakulima juu ya matumizi sahihi ya miradi ya umwagiliaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi ya zana za kisasa; mpaka sasa sehemu kubwa ya wakulima wanatumia zana butu na za kizamani katika kilimo hivyo kuathiri uzalishaji. Hali hii imepelekea uzalishaji mdogo na hivyo kusababisha ukosefu wa chakula na pesa kwa wakulima.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Wizara iweke masharti nafuu kwa kushirikiana na makampuni binafsi ili kukopesha matrekta kwa wakulima tofauti na urasimu uliopo sasa. Elimu itolewe kupitia Maafisa Ugani huko vijijini, ajira na semina za mara kwa mara zitolewe kwa Maafisa Ugani na Wakulima wakubwa katika maeneo ya vijijini. Bajeti ya Wizara ielekeze nguvu kwa kununua vyombo vya usafiri mfano, baiskeli, pikipiki magari kwa wataalam wetu ili waweze kusaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mifugo; kumekuwa na migogoro mikubwa kati ya wakulima na wafugaji kutokana na ongezeko kubwa la mifugo na mahitaji ya chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri bajeti ielekezwe katika kufanya mipango bora ya matumizi ya ardhi, hii itaepusha migogoro. Serikali itenge maeneo mapya kwa ajili ya shughuli za wafugaji na wakulima. Elimu ya uvunaji wa mazao ya kilimo na mifugo ifanyike mara kwa mara ili kupunguza idadi kubwa ya mifugo. Kufufuliwa na kuanzishwa kwa ranchi mpya ili kuendeshea ufugaji wa kisasa. Rushwa na vitendo viovu vidhibitiwe dhidi ya wafugaji na wakulima hali hii itapunguza migogoro kwa sababu haki itakuwa imesimamiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kuwa, mfumo wa usambazaji upitiwe upya na pembejeo ziwafikie wakulima mapema. Bei ya pembejeo ipunguzwe ili wakulima waweze kumudu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la stakabadhi ghalani. Kumekuwa na malalamiko mengi kwenye utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani hivyo kuathiri shughuli za kilimo Jimboni Nachingwea. Kero kubwa ni:-
(a) Kucheleweshwa kwa malipo ya kwanza, ya pili na bonus hivyo kuathiri shughuli za kilimo na kuwaingiza wakulima kwenye umaskini.
(b) Viongozi wa Vyama vya Msingi wakishirikiana na Maafisa Ushirika kuingia mikataba na wafanyabiashara wakubwa kuwaibia wakulima kwa kuwakata makato makubwa wakati wa malipo.
(c) Mabenki kutoza riba kubwa kwa Vyama vya Msingi, hivyo mzigo mkubwa kubebeshwa mkulima.