Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri na utekelezaji mzuri wa Ilani. Nawapongeza pia Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji kwa utendaji mzuri.

Mheshimiwa Spika, idadi kubwa ya wananchi wa Jimbo la Bagamoyo ni wakulima na wanaendesha maisha yao kwa kutegemea kilimo. Shida kubwa wanayopata wakulima wa Bagamoyo ni wafugaji wavamizi. Wafugaji wavamizi wamevamia karibu katika Kata zote za Jimbo la Bagamoyo, wanachunga ng’ombe mpaka katika mashamba ya wakulima bila kujali. Vyombo vya ulinzi na usalama Wilayani vimeshindwa kudhibiti uvamizi huo na wananchi wanapata shida sana.

Naiomba Serikali yangu tukufu iweke utaratibu wa kudhibiti wafugaji wavamizi. Naishauri Serikali iwaboreshee miundombinu ya ufugaji wafugaji hao katika maeneo wanakotoka.

Mheshimiwa Spika, ufugaji samaki ni eneo ambalo lina uwezo wa kuboresha lishe na ajira kwa Watanzania. Namuomba Mheshimiwa Waziri aweke mkazo na bajeti kubwa ya kutoa elimu ya kufuga samaki nchini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.