Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu uchapaji chapa wa ng’ombe. Uchapaji chapa ng’ombe unaharibu ngozi ya ng’ombe, hivyo itasababisha hasara ya ngozi ya ng’ombe. Naishauri Serikali waweke nembo kwenye masikio ya ng’ombe.

Mheshimiwa Spika, uchomaji nyavu moto unasababisha hasara kubwa kwa wavuvi. Naishauri Serikali badala ya kuchoma nyavu hizo, zingepelekwa VETA kwa ajili ya kuunganisha ili wapate nyavu inayotakiwa.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kamata kamata ya watu wanaoshikwa na samaki. Hii kamata kamata ya wanawake wanaokuwa na samaki hata wachache siyo haki. Naiomba Serikali waache kuwanyanyasa wanawake hao na badala yake waone ni namna gani watawadhibiti wavuvi haramu.

Mheshimiwa Spika, pia bado kuna tatizo kubwa la mifugo kuzunguka zunguka mijini. Naiomba Serikali iondoe mifugo mijini na iwatafutie wafugaji maeneo ya vijijini ambako kuna nyasi za kutosha. Pia naomba Serikali itoe elimu kwa wafugaji, wafuge kwa kutumia utaratibu wa zero grazing.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu bajeti ya maendeleo. Inasikitisha kuona kwamba pamoja na Wizara kutengewa bajeti ya maendeleo kwa mwaka 2016/2017 lakini kwa bahati mbaya fedha hiyo haikwenda kwa ajili ya maendeleo. Naiomba Serikali ihakikishe inafuatilia fedha yote tunayoidhinisha hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.