Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia, kama ifuatavyo:-

Kwanza napenda kuishauri Serikali kuangalia upya juu ya suala zima la upigaji chapa mifugo ambao unaharibu uzuri wa ngozi hivyo ngozi zetu kukosa soko katika soko la dunia.

Pili, napenda kushauri Serikali kujenga majosho ambayo miaka ya 1970 ilijenga majosho hayo na kusaidia wafugaji kuoshea ng’ombe au mifugo kwa kulipia kidogo hivyo kunusuru mifugo yao na magonjwa. Nashauri jambo hili lifanyike ili kusaidia wafugaji.

Tatu, nizungumzie suala zima la usalama wa nyama tunayotumia pamoja na machinjio yetu. Machinjio mengi nchini ni machafu, miundombinu yake ni mibovu na hatarishi kwa afya ya jamii. Nimetembelea machinjio ya Dodoma ni ya kisasa na safi. Je, kwa nini Serikali isiziagize Halmashauri zote nchini kujenga machinjio ya kisasa?

Nne, uchomaji nyavu za wavuvi si jambo la hekima bali kinachotakiwa ni kuzuia uingizaji au utengenezaji wa nyavu zisizofaa kufika kwa watumiaji.

Tano, operation ya uvuvi haramu iwe na weledi na si ya kuonea watu kwani tunajenga uhasama na jamii. Mfano, mwananchi ajue ni kiasi gani cha samaki anaruhusiwa kuwa nacho ili asiweze kushikwa siyo kama ilivyo sasa.