Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kwa maandishi kama ifuatavyo:-

(i) Uchomaji nyavu haramu; hatupingi operation za kuchoma nyavu lakini hoja ni kwa nini wavuvi ndiyo watu wa mwisho kuadhibiwa, nyavu hizi haramu zinaingiaje nchini? Nyavu zinapitaje na kuingia nchini? Endapo Serikali imeweza kudhibiti mahindi kuuzwa nje ya nchi inashindwa nini kudhibiti uingizwaji wa nyavu haramu nchini?

(ii) Kiwanda cha nyavu haramu Arusha, tuliona Waziri alifika katika kiwanda na kubaini utengenezaji wa nyavu hizi haramu. Je, ni hatua zipi Serikali imechukua dhidi ya kiwanda hicho? Kama wavuvi wakikamatwa na nyavu zinachomwa, je, kiwanda kilichozitengeneza kinachukuliwa hatua gani?

(iii) Migogoro ya wakulima na wafugaji Mkoa wa Morogoro bado ipo. Kwa nini Serikali isitafute suluhisho la kudumu? Kwa nini Ranchi ya Mkata, Kilosa ambayo imegeuka kuwa pori lisigawiwe kwa wakulima na wafugaji ili kukidhi upungufu wa ardhi na malisho kwa wakulima na wafugaji Wilayani Kilosa?

(iv) Usafirishaji wa ng’ombe toka Shinyanga hadi Dar es Salaam wanyama wanakufa njiani. Kwa nini Serikali isijenge kiwanda cha kisasa au machinjio ya kisasa wanapotokea ng’ombe na nyama ikasafirishwa magari yenye air conditioner na ikapelekwa Dar es Salaam badala ya ilivyo sasa? Kuendelea kusafirisha mifugo siku nyingi njiani ni kuwatesa mifugo na ni kinyume na haki za wanyama. Kama Dodoma kupitia machinjio yake wamesafirisha mbuzi toka Dodoma hadi Dar es Salaam na wamesafirishwa kwa ndege kwenda Uarabuni ndani ya saa 24, kwa nini Shinyanga, Kanda ya Ziwa washindwe kusafirisha nyama badala ya mifugo?