Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote sina budi kumshukuru Mungu kwa kunipa wasaa wa kuchangia kwa maandishi. Pia nampongeza sana Waziri, Mheshimiwa Mpina na Naibu Waziri Mheshimiwa Ulega.

Mheshimiwa Spika, Kibiti tuna ng’ombe wengi sana, kwa hiyo, naiomba Serikali yangu sikivu wafanye mazingira ya wafugaji yawe rafiki kwa kuwajengea malambo, majosho, machinjio ya kisasa, vituo vya minada na vituo vya kukusanyia maziwa. Kwa kufanya hivyo itatatua mgogoro baina ya wakulima na wafugaji kwani wananchi watafaidi kwa Halmashauri kukusanya ushuru na kuongeza kipato chake cha ndani hivyo kukamilisha miradi yake ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Kibiti ni Jimbo ambalo lipo pembezoni mwa Bahari ya Hindi ambapo kata tano, vitongoji 42, vijiji 17 vipo maeneo ya Delta na hivyo shughuli kubwa ya kujipatia kipato ni shughuli za uvuvi. Kwa hiyo, naiomba Serikali ituangalie kwa jicho la huruma.

Mheshimiwa Spika, uvuvi wa kamba mti, naomba yafuatayo yafanyike; kuongeza muda wa uvuvi (msimu); kubadilisha muda wa msimu, kwa sisi Wana Kibiti kamba mti wanapatikana kuanzia mwezi wa nane hadi wa 12; kupunguza wingi wa kodi; muda wa kuleta meli isiwe chini ya miaka 10, iwe zaidi ya miaka 20 na kuwasaidia wazawa kupata mikopo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ufugaji samaki, naomba Wizara ije na mpango mkakati wa kuanzisha uchimbaji wa mabwawa ya ufugaji wa samaki. Kwa kufanya hivyo, kutaongeza kipato, lishe bora, ajira kwa vijana na mapato ya Halmashauri.