Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naanza kwa kumshukuru Mungu aliyeniwezesha kuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nawashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Tumbatu kwa imani yao kubwa waliyonipa, kwa kunichagua kuwa Mbunge wao kwa kura nyingi sana. Natambua imani yao kwangu na nawaahidi kuwa sitawaangusha.
Tatu, natoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, kwa imani na uwezo mkubwa aliouonesha katika kulitumikia Taifa letu. Namwomba Mungu ampe kila jema katika uongozi wake huu.
Nne, napenda kumpongeza Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa pamoja na Baraza lake lote la Mawaziri kwa kuonesha uwezo mkubwa wa uongozi katika sehemu zao za kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uwezeshaji wa wavuvi na wakuzaji viumbe kwenye maji; katika sehemu ya ruzuku za zana za uvuvi, Serikali imetenga shilingi milioni 400 ambazo zilitumika kwa ununuzi wa zana za kilimo, zikiwemo mashine za boti. Pesa hizi ni kidogo sana kwa matumizi ya nchi nzima. Ushauri wangu ni kwamba Serikali iongeze kima hiki cha fedha. Aidha, Serikali iongeze mchango wake kutoka asilima 40 angalau kufikia asilimia 50 ambazo zitawawezesha wavuvi kununua zana hizo za uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri kwenye ukurasa wa 61, imeeleza kwa ufupi sana juu ya elimu ya maradhi ya UKIMWI. Nashauri kwamba elimu hii iongezwe kwa kiwango kikubwa ili kuwapa weledi zaidi wananchi juu ya ujinga na hatimaye kuepuka kabisa maradhi haya thakili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nahitimisha mchango kwa kuunga mkono hoja.