Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mungu kwa kuweza kuchangia Wizara hii muhimu ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Spika, Tanzania ni nchi ya tatu inayoongoza kwa idadi kubwa ya mifugo Barani Afrika. Bahati nzuri Wizara hii inachangia 4.4% ya pato la Taifa. Pamoja na kuwa na mifugo mingi bado haijitoshelezi mahitaji ya ndani na nje ya nchi mfano:-



NA. FAO TANZANIA
1. Nyama 50kg yr 11kg/yr – 0.03
2. Mazi wa 200 ltr/yr 45 ltr /yr– 0.013
3. Mayai – 300/yr 72/yr – 0.2.

Mheshimiwa Spika, FAO inataka kila Mtanzania atumie kilogramu 50 ya nyama kwa mwaka, lakini anatumia kilogramu 11 ya nyama kwa mwaka. Pia kila Mtanzania anatakiwa kunywa maziwa lita 200 kwa mwaka lakini anakunywa lita 45 tu kwa mwaka. Hata hivyo, kila Mtanzania anatakiwa ale mayai 300 kwa mwaka lakini anakula mayai 72 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, viwango halisi vinavyotakiwa kuzalishwa ni kama ifuatavyo:-


NA. FAO TANZANIA - UZALISHAJI
Nyama 50x50,000,000 (peoples) = 2,500,000,000 kg/yr 550,000,000 kg/yr
Maziwa 200x50,000,000 ltrs = 10,000,000,000 ltrs 2,250,000,000 ltrs
Mayai 300x50,000,000 = 15,000,000 /yr 3,600,000,000

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa FAO, Watanzania 50,000,000 kila mmoja anatakiwa kula 50 kg ya nyama, kwa hivyo Tanzania inatakiwa kuzalisha 2,500,000,000 kg/yr. Hata hivyo kwa mujibu wa FAO kila Mtanzania anatakiwa kunywa maziwa lita 10,000,000,000 yr kwa mwaka. Pia kuhusu mayai, FAO wanataka Watanzaia 50,000,000,000 watumie mayai 15,000,000,000 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika, hivyo Tanzania inazalisha mayai 3,600,000,000 kwa mwaka kwa mfano hai ni dhahiri kabisa kwamba mahitaji ya uzalishaji ni mdogo mno kulingana na mahitaji mengine. Kwa hiyo basi mambo yafuatayo ni lazima yazingatiwe:-

1. Kuzingatia ufugaji wa kitaalamu.
2. Kuwawezesha wafugaji kutunza mifugo yao kibiashara.
3. Kuimarisha malisho ya uhakika hasa wakati wa kiangazi.
4. Kuimarisha matibabu kwa mifugo yote nchini.
5. Kutenga maeneo maalum ya wafugaji.

Mheshimiwa Spika, hii itawezesha kuongeza kipato na pia kuongeza uzalishaji ili kutosheleza mahitaji ya watanzania lakini pia kuongeza pato la Taifa.