Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie machache katika hotuba ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Same Mashariki lina wafugaji wengi ambao bado wanafuga kienyeji. Wafugaji hawa walishatenga eneo kubwa kwa ajili ya kufanyiwa shamba darasa la jinsi ya kufuga kisasa na kupanda majani ya mifugo. Wilaya ya Same ina eneo takribani ekari 300,000 ambalo linafaa kwa ufugaji. Hivyo naomba Waziri awaeleze wananchi wa Jimbo la Same Mashariki, ni lini wataalam watafika jimboni hapo kuanzisha shamba darasa? Jambo hili nimeshapeleka ombi kwenye Wizara hii na Mheshimiwa Naibu Waziri Ole-Nasha alifika jimboni humu mwaka jana, lakini akashindwa kuwatembelea wafugaji hawa waliokuwa wamejiandaa sana kuonana naye.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili Jimboni Same Mashariki kuna bwawa kubwa lenye eneo la kilometa za mraba 24. Ziwa hili limejaa udongo na hivyo hata samaki hawawezi kuzaliana.

Mheshimiwa Spika, UNCDF walikuwa tayari kuanzisha mradi mkubwa kwa kutumia cages. Maandalizi yote yalikwishafanyika pamoja na kuweka muundo wa PPP, Halmashauri ya Wilaya ya Same ikishiriki kikamilifu. Lakini kutokana na tatizo hili la tope kujaa bwawani, wafadhili wanajaribu kuona jinsi ya kutengeneza mabwawa ya samaki nje ya Bwawa hili la Kalemawe lililoko Kata ya Kalemawe, Same Mashariki.

Mheshimiwa Spika, kwa vile Mito ya Hingilili na Yongoma inatiririsha maji yake kwenye hili Bwawa la Kalemawe, kutolitumia ni hasara kubwa kwa nchi yetu maana matokeo yake bwawa hili litakufa.

Naomba Waziri akihitimisha hoja yake anieleze jinsi atakavyoweza kusaidia ili bwawa hili lenye samaki linaweza likatolewe tope ili liweze kuleta kiwanda cha kuchakata samaki. Ahsante.