Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mimi nimwombe sana Waziri wa Fedha pamoja na Waziri Mpina waangalie suala la usindikaji wa ngozi.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016/2017 tulisindika jumla ya ngozi 1,000,215 ambazo ziliipatia Serikali shilingi bilioni 34.7; mwaka 2017/2018 ikashuka ikaenda mpaka vipande 292 iliyozalishia shilingi bilioni 3.2. Kutoka kwenye shilingi bilioni 34 mpaka shilingi bilioni tatu, sasa tatizo ni nini? Hebu Serikali mkae kwa sababu ng’ombe ni haohao, tatizo ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kutoka shilingi bilioni 34 mpaka shilingi bilioni 3 kwa mwaka mmoja na sisi Serikali tunatafuta pesa ili zikafanye kazi nyingine. Niiombe sana Wizara ya Fedha kama liko tatizo la tozo au export levy, hebu mkae na mtazame kwa sababu tunapoteza mapato mengi sana. Inawezekana ngozi hizi badala ya kupitia kwenye utaratibu wetu mzuri zinapitia Kenya na Uganda, hebu litazameni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili, nishauri sana, ukitazama kelele zote hizi zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge wanaosababisha hasa ni wataalam wetu, wanatuangisha mno. Bajeti zote ukisikiliza, kwa sababu wana tabia nzuri sana ya kusema kwamba aah, Mawaziri si wa kupita tu, walishapita wangapi hapa bwana, hawa ni wapitaji tu hawa, kwa hiyo, wanafanya mambo yao. Sasa kwenye haya ndugu zangu naomba tubadilike kwa sababu kelele hizi siyo zetu sisi peke yetu humu, ni mpaka na wapiga kura wetu huko. Kwa hiyo, niombe sana wataalam wetu maana hata ukitazama hiki kitabu, kimesemwa na wenzangu hapa, Mheshimiwa Ulega kakamata lile chuma anachoma ng’ombe ambaye hajawahi kufuga ng’ombe hata mbuzi. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, lakini ukija ukurasa wa mwisho wa kitabu chao, mtaalam ambaye ni daktari wa mifugo, Dkt. Maria na yeye kakamata chuma anambabua huyo ng’ombe. Tunataka kuuza ngozi, sasa mnaharibu ngozi. Kwa nini usitumie utaratibu wa kuchukua tag mkatoboa sikio, ndio utaratibu wa nchi zote duniani, mimi sijaona duniani wanachukua chuma wanamtoboa ng’ombe kwenye mapaja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi niombe sana wataalam wetu mliangalie hili. Mheshimiwa Mpina, tunajua wewe ni mchapa kazi mzuri sana, mdogo wangu, fuata mambo mawili katika maamuzi yako, pamoja na sheria, tumia busara na hekima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.