Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii muhimu. Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kunipa uhai na nguvu za kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa. Pili, nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anazozifanya kuendelea kuijenga nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo ambalo napenda kulizungumzia ni kuhusu hii operation inayoendelea. Mheshimiwa Mpina mimi naamini unafanya kazi nzuri na historia yako kila mmoja anaijua. Waheshimiwa Wabunge wamechangia mambo mengi niombe uyazingatie.

Mheshimiwa Spika, operation hii uliianzisha kwa nia njema lakini naamini kwa michango ya Waheshimiwa Wabunge baadhi ya watendaji wako wanakuangusha. Wana nia mbaya ya kutaka kuharibu lile zuri ambalo umeliandaa ili lisiweze kufanikiwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mpina ushauri wangu ninaokushauri, hebu fuatilia maoni ya Wabunge, baadhi naamini ni mazuri yanaweza kukusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine ambalo napenda kulisema kwa Waheshimiwa Wabunge, tumekuwa na hoja zinajitokeza hapa Bungeni, linapotoka jambo linafanyika Mheshimiwa Mbunge anasimama anasema wapiga kura wangu. Mimi nikuombe Mheshimiwa Mpina, simamia sheria, fuata taratibu, kile ambacho kinamgusa mwananchi ambaye hakufuata taratibu lazima twende kwenye mstari ulio sahihi. Nchi hii imefika hapa tulipo, mimi ninalisema hili, mimi ni mwanasiasa, lakini mambo mengi yamechangiwa na wanasiasa. Hata kama mtaona ni baya lakini wanasiasa tumehusika kuharibu nchi hii. Ukitaka kugusa hapa wanasema wapiga kura, ukitaka kugusa hapa hao watu wangu, mambo mengi ambayo yameharibika sisi ndiyo tumesababisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshauri Mheshimiwa Mpina jambo lingine, hili suala la ng’ombe kuchomwa moto kwa kweli siyo zuri. Hata kule kwangu nina ng’ombe wengi lakini wengine wana vidonda, yaani unajaribu kujiuliza hivi hawa ni wataalam ni watu gani ambao wametoa ushauri huu? Hili jambo sio sawa, angalia namna nyingine ambayo mnaweza kuwatambua hawa ng’ombe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine nikushauri Mheshimiwa Mpina, yako maeneo ambayo yalitengwa kwa ajili ya wafugaji lakini yamevamiwa. Kule kwangu kuna eneo limetengwa na Serikali likapewa GN. No. 620 ya mwaka 1987, eneo hili limevamiwa, wameingia watu wenye pesa, wameingia mpaka wengine kutoka nje ya nchi, wafugaji hawana pa kufugia wanahangaika. Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Mpina ulifuatilie hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.