Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii kuweza kuchangia Wizara hii muhimu ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Spika, naomba tu uniruhusu nisome kidogo baadhi ya vipaumbele katika sekta ya mifugo ambapo kuna kuimarisha usimamizi wa ardhi kwa kutenga maeneo ya malisho, kuimarisha upatikanaji wa maji na malisho ya mifugo, kuimarisha tiba na udhibiti wa magonjwa ya mifugo na kufanya sensa ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2015/2016 baada ya kuteuliwa kuwa Mbunge, nilipangwa katika Kamati ambayo ilikuwa ni kubwa kidogo kwa maana Kamati ya Kilimo, Mifugo pamoja na Uvuvi zikiwa pamoja. Vipaumbele ambavyo vinasemwa leo ni vipaumbele ambavyo vimekuwepo tangu mwaka wa kwanza kabisa mimi nimekuwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndani ya Bunge kipindi Wizara hii ipo pamoja bado haijatenganisha kulikuwa kumetokea ushindani wa aina fulani baina ya Wabunge kwa maana Wabunge wa Kilimo na Wabunge waliotoka katika maeneo ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais ametusaidia, amezitenganisha Wizara hizi. Hata baada ya kututenganisha tatizo limebaki kama lilivyokuwa tangu mwanzo nilipoingia katika Bunge hili. Mwaka wa kwanza kabisa 2016/2017 Serikali haikutenga pesa yoyote kwenda katika upande wa mifugo. Mwaka 2017/2018 Serikali imetenga shilingi bilioni sita kwa maana ya shilingi bilioni nne upande mifugo na shilingi bilioni mbili upande wa uvuvi. Pesa ambazo hazijapelekwa mpaka leo hii tunajadili bajeti nyingine. Leo Serikali inatenga tena bajeti ya shilingi bilioni 12 kwa maana ya bajeti hii na nina wasiwasi kwamba pesa hizi vilevile zinaweza sizipelekwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kipaumbele cha kwanza kwamba kuimarisha usimamizi wa ardhi kwa kutenga maeneo ya malisho, tunashawishika Wabunge kuwaambia wananchi kwamba Serikali ni sehemu mojawapo ya migogoro kati ya wakulima na wafugaji. Serikali ni washirika moja kwa moja kuhakikisha kwamba wakulima na wafugaji hawawezi kupatana na mapigano yaendelee. Kwa sababu kama tunatenga pesa na Bunge linapitisha ili kazi iweze kufanywa na Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, kutenga maeneo ya malisho kwa ajili ya wafugaji na hilo halifanyiki, maana yake ni kwamba wanaoshiriki kuwaua wakulima, wanaoshiriki kuwaua wafugaji na Serikali imo miongoni mwao lakini wao ni background players katika mauaji hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ifike wakati sasa kwa sababu Serikali yenyewe inashiriki kwa nyuma katika mauaji haya, basi ione umuhimu wa kuona kwamba ni lazima pesa hizi ziwe zinatengwa ili kazi ambayo imepangwa kufanywa iweze kufanywa. Tunaongea kifua mbele kwamba Wizara imekusanya maduhuli shilingi bilioni 21 kutoka kwenye mifugo, lakini tukiangalia kwamba wamewasaida nini hao wafugaji mpaka kwa hizo tozo wanazozitoa, hakuna lolote ambalo linafanyika kuweza kuwasaidia wafugaji.

Mheshimiwa Spika, kwa tozo ambazo zipo kwa maana ya leseni za biashara, tozo za kusafirisha ng’ombe, tozo za kulipia kila ng’ombe wanapokuwa wakihama katika eneo moja kwenda lingine ni vizuri sasa hizo kodi zikapunguzwa, kwa sababu kama mtu humsaidii katika kuhakikisha ya kwamba anakuwa na mazingira bora ya kuweza kuwatunza wale ng’ombe wake, ni muhimu sasa Serikali walau ikapunguza maumivu kwa hawa wafugaji ili kuhakikisha kwamba wanaweza walau wakaendelea bila ya tozo hizi za manyanyaso.

Mheshimiwa Spika, katika kilimo Serikali ilipunguza tozo na sasa Serikali iangalie pia namna ya kuweza kupunguza tozo ambazo zinawakabili wafugaji ili na wao kwa kile walichonacho basi washiriki katika kusaidia mifugo yao na wao wenyewe badala ya kuendelea kuilipa Serikali.

Mheshimiwa Spika, nitaongelea pia kidogo suala ambalo ameliongelea Mheshimiwa Balozi Dkt. Diodorus Kamala. Suala hili pia ni tangu Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akiwa Waziri wa Wizara hii yote kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, ndani ya Kamati Serikali ilitoa ahadi ya kwamba inafanya mchakato wa kuhakikisha kwamba ranchi zote ambazo ziligaiwa kwa watu zamani, ambazo hazifanyi kazi ziweze kurejeshwa na watu wengine wapatiwe ili maeneo ya kufugia ng’ombe ziweze kupatikana. Suala hili sasa ni miaka mitatu halijatimia Wizara ni hii tumeendelea kuongea mpaka mwisho hakuna linalofanyika, kwa sababu tu Serikali inashindwa kutoa hela. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ifike mahali sasa hawa wananchi ambao Rais anawaita anawapenda ni maskini, hebu tuwepende kwa vitendo kwa hela kupatikana ili kuboresha mazingira ya wananchi waweze kuwa vizuri. Ahsante sana.