Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, mimi niendeleze alipoishia Mheshimiwa Bulembo. Hadithi iliyopo ni kwamba nyavu ziko za aina mbili; ya dagaa na ya sagara.

Mheshimiwa Spika, nyavu za dagaa kapewa mtu mmoja Arusha kwa njia ya ajabu ajabu. Nyavu hizo zikiingia majini mwezi mmoja, zinakatika. Matokeo yake wafanyabiashara wanaagiza nyavu kwa njia ya panya, Serikali inakosa mapato, Mheshimiwa Waziri anajua, lakini yuko kimya, hakuna hatua iliyochukuliwa.

Mheshimiwa Spika, nyavu za sangara zimechukuliwa madukani, zimechukuliwa kwa wavuvi, zimechomwa, nyavu zimeagizwa na wafanyabiashara bandarini, hairuhusiwi kutoka kwa sababu yuko mfanyabiashara amepewa ili yeye ndiyo auze hizo nyavu. (Makofi)


Mheshimiwa Spika, zaidi ya hayo, watu wanateseka, wananyang’anywa pesa zao, shilingi milioni 20, risiti inaandikwa shilingi milioni tano. Kwa hiyo, naungana na Mheshimiwa Bulembo kwamba lazima operation hii isimame na uchunguzi ufanyike kwa sababu kuna harufu ya rushwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Bulembo amesema vizuri, hii ni Wizara ya siasa kama ilivyo kilimo na maji, ni Wizara za siasa. Mheshimiwa Rais amenunua Bombadier, sawa; anajenga reli, sawa, lakini wananchi wa kawaida Wizara hizi zitawaondoa madarakani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo napenda kuzungumza ni kuhusu Vituo vya Uhamilishaji. Mwalimu Nyerere alianzisha Vituo vya Uhamilishaji hasa maeneo ambayo sisi tuna zero grazing. Vile vituo vimekufa sasa hivi na matokeo ya vile vituo kufa, in-breeding ni kubwa na in- breeding inasababisha magonjwa, inasababisha ukuaji mbaya wa mifugo na maziwa kupungua. Naiomba Wizara ieleze mkakati wa kurejesha vile vituo ili kupata madume bora ya ng’ombe na mbuzi ili kuongeza kipato cha wananchi kwa njia ya maziwa na nyama.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ambalo napenda kulisemea kwa dakika zangu hizo ni kuku. Akina mama wengi wamesomesha watoto wa nchi hii kwa miradi ya kuku wa kienyeji na hao tunaoagiza, lakini hakuna chochote kilichosemwa na Wizara kuhusu mkakati uliopo wa kuendeleza ufugaji huu wa kuku.

Mheshimiwa Spika, ni kwamba hata ulaji wa mayai katika nchi hii umepungua kuanzia kwa watoto mpaka watu wazima na kwa sababu hiyo, lishe hii ambayo inahitajika sana kwa vijana wetu imepungua. Naomba Wizara ikija hapa ieleze mkakati ambao itatumia kuendeleza kuku na hasa kuku wetu wa kienyeji ambao wanapotea kidogo kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri akija hapa vile vile atueleze, ule ukatili uliofanywa Namanga wa kuchoma


vie vifaranga vilivyotoka Nairobi ni kwa sababu gani? Maana tuna sheria inayolinda wanyama. Vifaranga wamechomwa hadharani, ni uharibifu wa mazingira, ni ukatili, ni kuhatarisha mahusiano na wenzetu wa kutoka nje na kadhalika. Mheshimiwa Waziri atueleze, waliofanya ukatili ule wamechukuliwa hatua gani? Ili jambo hili lisipite hivi hivi bila kusemewa.

Mheshimiwa Spika, la mwisho ambalo ningependa kulizungumza ni kuhusu viwanda vya ngozi. Tulipandisha export levy hapa ya ngozi kwenda kwenye 8%, matokeo yake sasa hivi machinjio mengi wananchi wakipeleka ng’ombe zao wanaambiwa ondoka na ngozi; na pa kuipeleka ngozi hakujilikani. Ngozi zinaoza, zinanuka kwenye machinjio, Wizara ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba ngozi za nchi hii zimetumika kwa ajili ya kukuza uchumi katika Taifa letu?

Mheshimiwa Spika, kiwanda cha ngozi, kwa mfano Kanda ya Kaskazini, kile cha Himo pale hakitoshi kuchukua ngozi nyingine zote. Tumezungumza habari ya viwanda.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Wizara ilete mkakati wa namna ambavyo ngozi italiingizia hili Taifa pato na kuondoa adha ambayo wananchi wanapata kwa sababu ya ngozi.

Mheshimiwa Spika, nimalizie tu kwa kusema kwamba kero hizi ambazo tunazizungumza ni kero za wananchi.