Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzito walioifanya katika Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia tu kwa haraka haraka huwezi kujua kazi wanayoifanya Waheshimiwa hawa wawili. Leo hii kwa mfano nchi nzima kuwe hakuna nyama nchi nzima, hakuna maziwa, hakuna samaki utaona umuhimu wa Wizara hii. Wizara hii ni nyeti sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi Wizara hii pia inachangia kwenye Pato la Taifa kwa kiasi kikubwa kuliko Wizara nyingine nyingi. Kwa masikitiko makubwa, wanapelekewa bajeti ndogo. Ukiona kwenye maelezo ya Mheshimiwa Waziri, wamekusanya sana kwenye maduhuli. Sasa yale makusanyo waliyokuwa wanakusanya kwenye maduhuli, mengine yangekuwa yanarudi kwenye bajeti zao ili ziwasaidie kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi Wizara hii imetoka kwenye utaratibu wa kufanya identification ya ng’ombe walioko hapa nchini kwa kuwapiga chapa. Tuna ng’ombe takriban milioni 29 na kila mchangiaji alikuwa anatoa shilingi 500/=. Kwa hesabu ya haraka haraka tu, wamekusanya karibu shilingi bilioni 14. Tujiulize ni kiasi gani cha pesa kinarudi kwa ajili ya kusaidia kwenye sekta hiyo ya mifugo?

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo la msingi sana. Kwa hiyo, collection inayopatikana katika maeneo yao, tungetengeneza utaratibu wa kuhakikisha fedha zinarudi kwa ajili ya kuwasaida wakulima pamoja na wavuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo pekee ambalo linatoa ajira kwa urahisi ni eneo la uvuvi. Una-invest mara moja lakini una uhakika wa kufanya miaka yote katika eneo hili. Wizara inatakiwa itambue hilo; na kuwa karibu sana na kuwashirikisha sana katika kazi zao sekta binafsi.

Mheshimiwa Naibi Spika, miongoni mwa mambo yaliyolalamikiwa na Wabunge wengi ni mahusiano kati ya Wizara, pamoja na sekta binafsi. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Waziri alione hili gap alipunguze. Kuna watu wanataka wakae, wazungumze pamoja kwa ajili ya maslahi ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni eneo la tasnia ya maziwa. Tuna viwanda vikubwa vitano katika nchi hii. Tuna takwimu ya ng’ombe milioni 29 ambao nimezungumza. Kwa masikitiko sana, asilimia 85 ya maziwa yanayotumika hapa nchini yanatoka nje ya nchi. Sasa tujiulize, huu wingi wa ng’ombe unasaidia nini katika tasnia ya maziwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanaogopa ku- invest katika eneo hii kwa sababu ya tozo mbalimbali zilizopo ambazo hazina tija kwa watu wetu. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri, zile tozo ambazo hazina tija, tuziondoe kusudi watu waweze kujiunga katika maeneo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni ku-protect viwanda vya ndani. Wewe ni shahidi maofisi yote ya Serikali yanatumia maziwa kutoka nje. Ukienda kwenye ofisi yoyote hapa au majumbani utakuta Nido au Lactogen kutoka nchi za nje. Kwa nini tusitumie maziwa ya ndani? Kwa utaratibu huu, tunaendelea kuvidhoofisha viwanda vya ndani badala ya kuvisaidia. Kwa hiyo, ifike wakati tuweke ban kama tulivyoweka ban kwenye furniture kwamba sasa ni marufuku kuagiza maziwa nje, tutumie maziwa yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache, naunga mkono hoja.