Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwa maandishi, kwanza ni kuhusu pembejeo za kilimo. Wizara imeshindwa kusimamia utaratibu wa ugawaji pembejeo za wakulima kwa wakati badala yake imekuwa kilio na kupata pembejeo za kilimo kwa kuchelewa ikizingatiwa kuwa wakulima wengi hawana uwezo wa kumudu gharama kubwa za mbolea na wanategemea mbolea ya ruzuku ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ikiri wazi kuwa mfumo wake wa kupatia wananchi mboleo ume-fail na watafute mbinu nyingine ya kufikisha mbolea hizo kwa wakulima kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masoko ya uhakika wa mazao bado. Bado kuna changamoto, Serikali imekazana kudhibiti uuzwaji wa mahindi nje ya nchi huku Serikali ikishindwa kuwa na mfumo mbadala wa kusaidia wananchi wake kuuza mazao yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao ya mahindi yameharibika, wananchi wamepata hasara ikiwemo Mkoa wa Morogoro. Serikali imewaweka wananchi katika mazingira magumu sana wengine kupata hasara. Cha kushangaza, mahindi kutoka Zambia yanapita Tanzania na yanaenda Kenya kuuzwa, hiyo siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya mawakala wa pembejeo za kilimo ambao wamefanya kazi ya kupeleka huduma kwa wakulima mpaka sasa hayajalipwa. Hii ni aibu na uonevu kwa wakulima. Serikali iliahidi kupitia madai yote na kubaini madai hewa na halali, mpaka sasa hamna majibu. Tatizo hili kama Serikali haitatenda haki kwa mawakala halali, hii itaendelea kujenga chuki kati ya Mawakala na Serikali yao. Ni vyema Serikali ikapitia upya madai hayo na kutoa haki kwa mawakala.