Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuchangia machache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo tunacholima Watanzania siyo chenye tija. Wakulima wengi wanalima kwa mazoea, siyo kama biashara ya kuwapatia kipato.

Mheshiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tanga kuna Kituo cha Utafiti cha Kilimo kilichopo Mlingano Wilaya ya Muheza. Kutokana na kituo hiki, wakulima hawapati msaada wowote kutokana utafiti wa udongo wa mazao yanayostahili kulimwa katika eneo hilo. Ombi, kwa nini Mheshimiwa Waziri asihamasishe umuhimu wa kupima udongo na kuelewa aina ya mazao yanayoweza kustawi katika maeneo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mikoa ya Pwani ni maarufu kwa kilimo cha minazi. Minazi ikivunwa ina manufaa sana. Mafuta ya nazi ni mazuri sana, hayana lehemu. Mheshimiwa Waziri atueleze, ni lini Tanga kutaanzishwa kiwanda cha kutengeneza mafuta kutokana na nazi zinazovunwa Tanga, Pangani, Mkinga na Muheza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya 1960 sekta binafsi waliweza kutengeneza kiwanda cha kukamua mafuta ya nazi. Kiwanda hiki kilikuwa katika Jiji la Tanga. Mafuta yaliyozalishwa hapo yaliitwa Nicolin. Wananchi walitumia mafuta hayo kupikia vyakula mbalimbali na wala hayakuleta madhara kwa walaji. Tunaomba Serikali itujengee kiwanda cha kusindika mafuta ya nazi.