Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu sekta ya kilimo inabebea asilimia 65.5 ya Watanzania ni lazima Wizara itoe kipaumbele ili kutoa au kupunguza umaskini kwa wakulima na kuongeza pato kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukuaji wa kilimo hauridhishi hata kidogo, inasikitisha tangu tupate uhuru mwaka 1961 huu ni mwaka wa 57 bado kilimo kinasuasua. Ili kupunguza umaskini ilikuwa ni lazima kilimo kikue kuanzia asilimia 8 hadi 10 hadi sasa. Huu ni mwaka wa 57 kilimo kinakua kwa asilimia 2.7 hadi 3.0. Ni lini tutapunguza umaskini wakulima wetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, uelekezaji katika kilimo, Serikali bado haijaamua na kuonesha nia ya kupunguza umaskini kwa wakulima; bajeti inapungua kila uchao. Inasikitisha kuona nchi kama Rwanda imewekeza jumla ya dola bilioni 32 na Tanzania kushindwa kufanya uwekezaji wa kuwapunguzia wahusika umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tuwe na tahadhari na umakini mkubwa katika kilimo. Jambo la kwanza ni lazima kuwa na watafiti wa kutosha kuwa na vyombo vya kilimo kama tractor na power tillers, kutumia ardhi kitaalam; kwa mfano tunazo hekta 1,955,270 zinazohitajika kulimwa. Hata hivyo jambo la kusikitisha ni hekta 13,915 zimelimwa na tractors na power tillers.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko hekta 3,404,494, hizi zinalimwa na wanyama na hekta 8,560,517 zinalimwa kwa jembe la mkono. Kwa takwimu hizi ni wazi kwamba Wizara ya Kilimo haijajiandaa kwa ajili ya kupunguza umaskini kwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhuru wa wakulima, wakulima lazima wapewe uhuru wa kuuza mazao yao yote. Kama Serikali wanahitaji basi iweke mazingira ya soko la ndani ili wakulima waweze kuuza mazao yao na kupata faida.