Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia pia katika Wizara ya Kilimo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, masoko bado ni changamoto kubwa kwa wakulima hapa Tanzania. Tanzania imezidi kuwa nyuma katika udhibiti wa masoko ya mazao ya kilimo kutokana na masharti magumu ya usafirishaji nje ya nchi. Hata katika taarifa ya Benki ya Dunia (WB) nchi yetu inaonekana ipo nafasi ya 56 kati ya nchi 62. Hii inasababishwa na ugumu wa kupata vibali vya kusafirishia mazao hayo nje ya nchi hii. Kwa Tanzania inachukua hadi siku zaidi ya 20 ili kukamilisha tararibu zilizopo ili kuweza kupata vibali wakati kiutaratibu kwa nchi zilizizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara zinahitajika siku si zaidi ya sita kufanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naishauri Serikali ikazane kupunguza vikwazo kwenye upatikanaji wa vibali vya kusafirishia mazao nje ya nchi ili wakulima wa Tanzania pia waweze kufaidika na sekta hii ya kilimo. Uchumi wa Tanzania utatengemaa zaidi kama sekta ya kilimo itakuwa nzuri. Tukumbuke wakazi wengi wa Tanzania wanaishi vijijini na huko ndiko msingi wa kilimo ulipo. Wakulima wengi wanalima na kuishi vijijini, lakini cha kushangaza huko ndiko kuna matatizo kila siku. Kama uchumi kupitia kilimo ungekuwa mzuri hata maisha ya wananchi waishio vijijini yangekuwa na ahueni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uzalishaji wa mazao ya mbegu za kilimo nchini bado ni changamoto kubwa. Nasema hivyo kwa sababu Serikali imetumia pesa nyingi sana kufanya uzalishaji huu lakini wakulima wengi hawana taarifa au hawajapata elimu ya kutosha kuhusiana na mbegu hizi ambazo nyingi sifa yake kubwa ni kuhimili ukame na kuzalisha mavuno mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Wizara ya Kilimo kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima wa Tanzania ili mbegu hizi ziweze kutumika na hatimaye kuongeza kipato pamoja na mavuno mengi ya mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo makubwa ya ardhi yanamilikiwa na wakewezaji wachache, hii ni kwa ajili ya wakulima wadogo wengi kukosa kipato cha kutosha cha kumiliki ardhi na hivyo kukosa ardhi ya kutosha ya kufanya kilimo. Ugawaji wa ardhi umekuwa ukifanyika bila kumilikisha wenyeji wa maeneo husika na kusababisha tatizo kubwa la migogoro ya ardhi ambavyo hata Serikali imeshindwa kutatua katika sehemu nyingi hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuhusisha wenyeji wa maeneo husika wakati wa kumilikisha na kununua ardhi ili kutoa haki kwa kila mtu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo kubwa katika utoaji wa mikopo nchini, wakulima wadogo wadogo wamekuwa wakikosa fursa ya kupata mikopo katika taasisi mbalimbali za kifedha ili waweze kuwekeza kwenye kilimo, na hii inatokana na wananchi wengi kutokuwa na hatimiliki ya ardhi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri na kuisisitiza Serikali kupeleka mikopo kwa wakulima wadogo hasa wa maeneo ya vijijini ambako ndiko wakulima wengi walipo.