Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wakulima wa korosho kuuza korosho zao katika minada tangu mwezi Novemba, 2017 mpaka leo hawajalipwa fedha zao linasababisha wakulima hawa kukosa fedha kwa ajili ya kujikimu, kusomesha watoto wao na pia kuandaa mashamba kwa wakati kwa ajili ya msimu wa mwaka huu. Je, Serikali imeshindwa kulisimamia suala hili ili wakulima hawa wapate fedha zao kwa wakati kwa ajili ya kutatua shida zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa mbegu bora za mazao mbalimbali unasababisha wakulima kupata mavuno kidogo ikilinganishwa na nguvu inayotumika kulima kwa sababu tu ya kukosa mbegu bora. Pia hata zikipatikana basi bei inakuwa kubwa sana ambayo mkulima wa kawaida anashindwa kumudu kununua. Ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wakulima wa mazao mbalimbali hapa nchini wanapata mbegu bora kwa ajili ya kufanya kilimo chenye tija?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kilimo cha umwagiliaji kinaleta tija? Mfano katika Mkoa wa Mtwara kuna bonde kubwa katika Kata ya Kitere, Mtwara Vijijini ambalo kama lingetumiwa vizuri lingesaidia uzalishaji wa kutosha wa zao la mpunga na kuwawezesha wananchi kujipatia chakula na kipato. Pia bonde hilo lingewezesha kulima mboga mboga kwa ajili ya biashara na matumizi mengine ya kifamilia. Ni nini mkakati wa Wizara utakaoleta tija kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara wenye mabonde yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, kama vile Kitere, Mahurunga na Ruvuma?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata ufafanuzi juu ya madeni yanayodaiwa na mawakala waliosambaza pembejeo za kilimo, kwa sababu kuna kauli zinazochanganya kutoka upande wa Serikali na mawakala, nani ni mkweli? Mawakala wanasema wanadai madai halali wakati Serikali inasema mawakala waongo. Je, Serikali imebaini nini baada ya kufanya uhakiki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali imeshindwa kutoa bure pembejeo ya zao la korosho, ikizingatiwa kwamba zao hili linachangia pato la Taifa hili la Tanzania?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo la wakulima wa korosho kucheleweshewa malipo yao yaliyopitia benki, kwa hiyo nashauri Serikali kuzitaka benki kuwalipa wakulima mara moja pindi tu wanunuzi wanapolipa hela za wakulima.