Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya bajeti ya Waziri wa Kilimo na maoni ya Kamati. Kilimo ni uti wa mgongo, kauli hii haiendani na utekelezaji kutokana na changamoto zifuatazo;

Kwanza, kutopewa kipaumbele kwenye bajeti kwa kutengewa fedha kidogo zisizoweza kukidhi uhitaji wa utekelezaji wa yale yanayopaswa kutekelezwa.

Pili, kutopewa fedha yote iliyotengwa pamoja na uchache wake kunachangia kukwamisha Wizara hii kutekeleza majukumu yake na tatu, kutokuwa na Maafisa Ugani wa kutosha huko vijijini ambao wangeweza kuwasaidia wakulima kulima/kupanda mbegu bora/kupalilia na kuvuna mazao kwa lengo la kujiinua kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, vyuo vya utafiti kutopewa fedha za kutosha kufanya utafiti wa mbegu ili wakulima waweze kupanda mbegu bora na yenye kuwawezesha kuvuna mazao ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, uwepo wa migogoro ya ardhi kunachangia kwa asilimia 50 kati ya wakulima na wafugaji kukwamisha juhudi za wakulima kujipatia mazao ya kutosha kutokana na wafugaji kulisha mifugo kwenye mazao yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuishauri Serikali kama ifuatavyo:-

Kwanza, Serikali ina mpango mzuri wa nchi yetu kuwa ya viwanda na kilimo ndicho kitakachotoa malighafi zitakazolisha viwanda hivyo. Ni vema bajeti ya kilimo iangaliwe upya na kupewa kipaumbele cha juu ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yake vizuri na Tanzania ya viwanda itawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, bajeti wanayotengewa wapewe yote kulingana na umuhimu wa majukumu yao yatakayowezesha na kuandaa Tanzania ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Serikali itoe ajira za wagani maeneo /vijiji ambavyo hawana watumishi wa fani hii waweze kupelekwa na kuwawezesha vitendea kazi, ili waweze kutenda majukumu yao kikamilifu. Vyuo vya utafiti viwe na bajeti ya kutosha ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakamilishe kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji ili wananchi hawa kila mmoja waweze kuishi kwa amani na shughuli za uzalishaji ziweze kufanyika kwa uhakika zaidi. Naomba kuwasilisha.