Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya tatizo kubwa na sugu linalofanya uzalishaji wa korosho katika Mikoa ya Kusini ni uzee wa miti iliyopo. Kama ilivyo katika mazao mengine kama miembe, michungwa, parachichi, limao na mengine mengi ni wakulima wachache sana wanazalisha mazao hayo kibiashara wanatumia miche au miti ya zamani ya kiasili. Wengi wanatumia ya kisasa (cross breed) ili kuweza kupata mti bora wenye uwezo mkubwa wa kuhimili magonjwa kutoa mazao mengi na kuweza kuzaa ndani ya muda mfupi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango gani ili kuhakikisha kwamba wakulima wa korosho wanapanda kwa wingi miche ya kisasa ya mikorosho inayozozalishwa nchini ukizingatia kwa muda mrefu zao la korosho limekuwa likishika namba mbili nyuma ya tumbaku katika mazao yanayoliingizia Taifa pesa nyingi pamoja na pesa za kigeni, kuna mashamba ambayo yameteuliwa kuzalisha miche ya mikorosho ya kisasa, mashamba hayo yapo Mkoa wa Tanga, Pwani na maeneo machache ya Mkoa wa Lindi na Mtwara. Serikali ina mpango gani wa kuinua uzalishaji wa mashamba haya ili miche inayozalishwa iweze kuwafikia wakulima wengi zaidi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine ni ufisadi uliokithiri, wawakilishi wa wanunuzi huhongwa katika minada badala ya kuwa upande wa wakulima wanakuwa upande wa wanunuzi pamoja na viongozi wa vyama vya msingi. Hii hupelekea wote kwa pamoja kushirikiana katika kumkandamiza mkulima na kumfanya mnunuzi anaeshinda kununua sio anayetoa bei ya kumnufaisha mkulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine lipo katika mfumo na mlolongo mzima wa malipo kuwa mlolongo mrefu sana kupelekea pesa kuchelewa kumfikia mkulima na kupelekea wakulima waone bora kuuza korosho kwa njia ya kangoma kuliko kupeleka korosho zao kwenye utaratibu wa stakabadhi ghalani. Malipo hupitia process ambazo ni manual na taratibu za kibenki kuchukua muda mrefu kiasi cha kwamba hadi pesa inamfikia mkulima inakua tayari imeshuka kwa mfumo thamani. Serikali ijitahidi kuhakikisha kuwa mfumo huo unafupishwa ili kuweza kutoa nafasi kwa mkulima kupata pesa zake kwa wakati na kufanya maandalizi ya msimu unaofuata mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuzungumzia suala la utawala mbovu katika Wizara ya Kilimo. Wafanyakazi wengi wamesimamishwa kwa muda hadi kufika mwaka mmoja na zaidi bila kupewa nafasi ya kusikilizwa wala kuchunguzwa jambo ambalo liko kinyume na taratibu za kisheria. Wengine walisimamishwa kwa kosa la kile tunachoita kutekeleza majukumu yao ya kazi mfano, TPRA ambao walileta taarifa kuwa mbolea iliyoingizwa nchini ilikuwa mbovu, iliamuliwa kwamba mbolea ikakaguliwe na Mkemia Mkuu ambaye alithibitisha kuwa mbolea haina matatizo lakini katika hali ya kushangaza mbolea hiyo hiyo ilipoingia kwa ajili ya matumizi ikaonekana na ikathibitika kuwa mbovu. Sasa
hao waliosimamishwa baada ya Mkemia Mkuu kuthibitisha kuwa mbolea ni nzima kwa nini baadae ilipothibitika kuwa kweli mbolea mbovu kwa nini hawajarudishwa kazini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni mfano mmoja tu lakini wafanyakazi wa vitengo mbalimbali wamesimamishwa kwa kipindi kirefu bila kujua hatma yao. Huu ni utawala mbovu ambapo haki za wafanyakazi hazisimamiwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa napenda kuzungumza juu ya makampuni na mawakala kuna madai ya mwaka 2014/2015, 2015/2016 hali kadhalika, lakini cha kushangaza kila siku Wizara inafanya ukaguzi na uhakiki wa madai hayo. Ifike wakati sasa watu walipwe madai yao. Wizara itueleza ni lini watalipwa madai yao.