Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kupata nafasi hii kuchangia hoja iliyopo mezani. Pamoja na kwamba kilimo ndicho kinachotoa ajira kubwa kwa Tanzania, bado bajeti inayotengwa kwa eneo hili ni ndogo sana. Hivyo ili kuleta mapinduzi ya kilimo mambo yafuatayo yazingatiwe:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itenge bajeti ya kutosha, Maafisa Ugani wapewe motisha kama pikipiki na watawanywe kwenye vijiji vyote, wakipewa malengo ambayo yatatumika kupima utendaji wao wa kazi. Uwepo mfumo unaoainisha kila Afisa Ugani anahudumia idadi gani ya wakulima wawe na majadala kwa kila mkulima na kufuatilia maendeleo yao, kama ilivyo kwa madaktari kwa uwiano wa daktari mmoja kwa wagonjwa10,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwepo uhusiano wa karibu kati ya Wizara ya Kilimo inayotoa sera na kusimamia kilimo, taasisi za mafunzo kama SUA na taasisi zingine za utafiti. Tafiti bora kwa mazao zifikishwe sasa kwa wakulima kwa mafunzo na mashamba darasa. Nchi zilizofanikiwa kwenye mapinduzi ya kijani, Serikali kupitia Wizara iligharamia mafunzo ya wakulima kwenye taasisi za utafiti ili kuhakikisha wakulima wanajifunza mbinu mpya za kilimo cha mazao mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mafunzo mashamba darasa huanzishwa kwenye vijiji ikisimamiwa na Maafisa Ugani, mashamba haya ndiyo hutumika kusambaza teknolojia ya uzalishaji kwa makundi mengi ya wakulima wadogo wadogo. Ni muhimu hii Wizara ya Kilimo ikapata msimamo wa Wizara ya Viwanda kujua ili viwanda gani vinavyozungumziwa ili Wizara ya Kilimo ijikite kwenye kilimo cha mazao ambayo yatahitajika kwenye viwanda vinavyoanzishwa. Uratibu wa Wizara zinazohusiana ni muhimu kuepuka mkanganyiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.