Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi nataka niseme mambo machache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka niwaombe Waheshimiwa Wabunge, bajeti hii tutumie Kanuni ya 69 tuirudishe ili Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha zikakae kuweza kuja na bajeti ambayo inagusa maisha ya watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitumie takwimu hizi. Tumeandaa bajeti ya shilingi trilioni 32, shilingi trilioni 12 ni fedha za maendeleo. Sekta ya kilimo inachangia almost 30% ya GDP ya nchi yetu, development budget ya sekta ya kilimo ni shilingi bilioni 94 ambayo ni sawasawa na almost 0.8 ya total budget ya maendeleo, kweli? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta inayochangia almost 30% ndiyo inatengewa chini ya asiliamia moja ya bajeti nzima ya maendeleo. Sekta ambayo inaajiri kati ya asilimia 60 mpaka 70 ya Watanzania ndiyo inatengewa chini ya asilimia moja ya bajeti ya maendeleo. Sekta ambayo ina-supply asilimia 70 ya viwanda vyetu inatengewa chini ya asilimia moja ya bajeti ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine la kusikitisha sekta hii imeendelea kuonewa katika nchi hii kwa muda mrefu na siyo sahihi. Sisi Wabunge, hasa wa Chama cha Mapinduzi, tuna wajibu wa kumlinda mkulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shinyanga, Tabora, Kigoma, Mwanza, Simiyu, Katavi, Mara, Rukwa na Ruvuma, huku kuna mkulima na mfugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikoa hii ndiyo inayolima mahindi, pamba, ndiyo yenye ng’ombe na samaki, halafu ndiyo watu tunaowatesa, it is unfair. Nadhani ni vizuri sisi viongozi wa nchi hii tukatambua hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Uislam Mwenyezi Mungu amemuumba mwanadamu kuwa Khalifa, kuwa kiongozi wa viumbe vingine. Mwenyezi Mungu kampa mwanadamu utu na akili ili aweze kuwatendea wema wengine, leo nyavu zinachomwa, leo mifugo ya nchi hii wafugaji wamekuwa wakimbizi, leo wakulima wa nchi hii wanaonewa, tunam-sacrifice huyo bwana aliyekaa hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano mdogo, ili mkulima aweze kulima mahindi heka moja anahitaji input zifuatazo; trekta kulima mara mbili anatumia shilingi 90,000; harrow atatumia shilingi 35,000; kupanda atatumia shilingi 30,000; kupalilia atatumia shilingi 60,000 in total; ili aweze kupanda mahindi anahitaji mfuko wa jumla ya kilo nane ambayo atatumia shilingi 45,000; bado ataweka mbolea ya kupanda na kukuzia, in total anatumia shilingi 550,000. Leo mahindi ni shilingi 150 kwa kilo. Cost per unit ya production yake ni shilingi 500, are we realistic? Turudisheni hii bajeti. This is not healthy for our country. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Tizeba hana problem kaomba 60 billion shillings kwa ajili ya inputs ya tumbaku. Tumbaku mwaka jana tumeteseka wananchi wa Mkoa wa Tabora. Leo tumeletewa pamba mtu anaitwa galagaja, galagaja kule usukumani ni middle man, huu ushirika ulioletwa kwenye pamba hauna mtaji. Ziara ya kwanza ya kiongozi wa ushirika, mmoja alienda Kishapu anauliza eti inakuwaje wafanyakzi wa SHIRECU hawalipwi mshahara, ninyi SHIRECU mna shamba? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri turudishe bajeti hii na mambo yafuatayo yafanyike. NFRA apewe fedha aliyoomba. Suala la pili, kusiweko na condition kusafirisha… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)