Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa ya kuchangia katika Wizara hii ya Kilimo ambayo ni muhimu kwa zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja, kwanza kabisa ni bahati mbaya sana sekta hii ya kilimo imekuwa haipewi kipaumbele. Asilimia zaidi ya 80 ya Watanzania ni wakulima na napenda niseme katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha wakati akiwasilisha ukomo wa bajeti alisema kwamba katika bajeti ya mwaka 2018/2019 bajeti hii imetoa kipaumbele katika mambo yafuatayo, nitayasema machache. Alisema kwanza kulipa deni la Serikali; pili, kugharamia ujenzi wa miundombinu pamoja na reli na viwanja vya ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweka kipaumbele katika vitu na si watu na ndiyo maana watu wanajiuliza, hivi mnavyosema uchumi umekua, umekua wapi? Mifukoni mwa watu hawana pesa, wakulima wanalima hawapati masoko ya mazao yao. Hawa wakulima sijui itakuwaje, mtawajibu nini mwaka 2020 kwa sababu mmewatelekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi katika Mkoa wangu wa Iringa wananchi wanalima mahindiambayo ndiyo zao lao la chakula na ndiyo zao lao kuu la biashara pamoja na mazao mengine yakiwemo alizeti, ngano, karanga, viazi na vitu vingine. Haya mahindi yalikuwa yanauzwa mpaka shilingi 80,000 kwa gunia mpaka shilingi 100,000 mwaka jana. Sasa hivi gunia la mahindi ni shilingi 25,000, debe moja ni shilingi 5,000 mpaka shilingi 4,000. Huyu mkulima amenunua mbolea kwa gharama kubwa sana mwishoni anakuja kuuza gunia la mahindi kwa bei ambayo hata nusu ya mfuko wa mbolea haifikii, hii haikubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukijigamba hapa tunakwenda kununua ndege ili wananchi wapande, wananchi wangapi wanaopanda ndege? Katika Mkoa wangu wa Iringa ukitaka kuhesabu wanaopanda ndege asilimia zaidi ya 90 hawapandi ndege. Tunaomba mkae mliangalie suala hili ili wananchi hawa waweze kupata fedha kwa kuwapatia masoko ambayo yatakuwa yanawasaidia wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika suala la mbolea. Mbolea zimekuwa haziji kwa wakati, sisi kule kilimo chetu msimu wetu unaanza Novemba amabo ndiyo mvua za kupandia zinaanza lakini inapofika Februari au Machi ndiyo mbolea zinakuja, hii mbolea itamsaidia nani? Tumewatupa watu wetu na hatuwapi mambo yanayostahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijawa Mbunge nilikuwa nasikia masuala haya ya kulalamikia bajeti ya Wizara ya Kilimo, ya kulalamikia jinsi ambavyo mawakala wanapata shida. Nimekuja nipo Bungeni mwaka 2015 hivyo hivyo, mwaka 2016/2017 hivyohivyo, naingia hii mwaka 2017/2018 bado suala la kulalamikia bajeti ndogo ya Wizara ya Kilimo iko vilevile. Tunaenda wapi na nchi hii? Tunakwenda wapi na Watanzania wanakwenda wapi? Mmesema tunataka tuwe na nchi ya viwanda, viwanda hivi vitapata malighafi kutoka wapi? Wakulima wamekata tamaa kabisa, hawana matumaini na Serikali yao... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)