Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie kwenye mapendekezo haya ya bajeti ya Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpa pole Kaka yangu Engineer Dkt. Tizeba nadhani hii kazi ni ngumu kidogo na pengine yako mambo yapo nje ya uwezo wake, naona toka jana shughuli imekuwa ngumu kidogo hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisikiliza mjadala huu toka jana kwa mara ya kwanza kuna dalili kwamba watu wengi hawaungi mkono haya mapendekezo, bila ya kujali pande zote na bahati nzuri kwa mfumo wetu wa bajeti tulionao iko room ya Serikali kwenda kuangalia upya, kwa sababu tunaanza na bajeti ndogo ndogo halafu tunakwenda kwenye bajeti kubwa. Kwa hiyo, ushauri wangu wa kwanza Mheshimiwa Waziri na Serikali tusione shida kukubali hali halisi kwamba ni vizuri tuende tukaangalie upya bajeti hii wala tusione taabu, ni jambo la kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira tuliyonayo kama trend yenyewe ndiyo hii, nataka kusema huu ni mtihani mkubwa sana kwa Serikali ya Awamu ya Tano kwenye hii bajeti. Kwa sababu ni hapa ambapo tutatakiwa kujipambanua tunajikita kwenye maendeleao ya vitu au maendeleo ya watu. Kama ni maendeleo ya watu bajeti hii ndiyo inagusa zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kelele unazozisikia Mheshimiwa Waziri kwenye pamba, kahawa, korosho na mbaazi ambayo mmetuambia tukale na maeneo mengine yote ni kwa sababu inagusa maisha ya watu. Sasa Serikali tunayo choice ya message tunayotaka kuipeleka kwenye umma. Message kwamba tunajali maendeleo ya vitu au tunajali maendeleo ya watu ambao ndiyo waliotuweka madarakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia trend mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali ilitenga asilimia 0.93 ya bajeti kwenye Wizara ya Kilimo, mwaka 2017/2018 ikashuka ikaenda asilimia 0.85, mwaka 2018/2019 haya mapendekezo ya sasa hivi tumeshuka tena tumekwenda asilimia 0.52 ya bajeti. Maana yake moja tu ni kwamba kila mwaka tunashusha bajeti tunayoitenga kwenye sekta ambayo ndiyo inagusa watu wengi kuliko wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, itakumbukwa hapa tuliwahi kupendekeza wakati fulani na tukashambuliwa kama vile siyo wazalendo, kama vile tuna chuki hivi, tulisema Serikali ni vizuri ikakwepa kuwekeza fedha za ndani nyingi kwenye miradi mikubwa ambayo inaweza kujiendesha kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kuendelea kushuka kwa bajeti muhimu kama ya kilimo ni kwa sababu tumeamua kupeleka fedha zetu za ndani kwenye kuwekeza kwenye miradi mikubwa ambayo ingeweza kujiendesha kibiashara, kwa hiyo madhara yake tutayaona tu. Inawezekana kweli tukaonekana siyo wazalendo lakini hivi ukweli huu unahitaji elimu gani kujua kwamba tunaendelea kushuka na mimi naamini hili kaka yangu Mheshimiwa Tizeba siyo lako, tutakubebesha mzigo ambao siyo wako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nimemsikia shemeji yangu Mbunge wa Ruvuma mpaka analia hapa, watu wanadai, watauziwa mali zao kwa sababu bajeti unayopewa ndogo huna namna. Hela inaenda wapi kama tumebana matumizi, hela inaenda wapi kama tunakusanya? Bahati mbaya rafiki zangu ushabiki unakuwa mwingi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa kwanza Serikali isione aibu kuipitia upya bajeti hii kwa sababu bajeti hii tukiipitisha kama ilivyo message kwa Watanzania ni mbaya sana kwa Serikali ya Awamu ya Tano kwamba tunataka kuwekeza zaidi kwenye vitu badala ya watu! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda ukaangalia hali halisi thamani ya mazao ambayo wananchi wetu wanazalisha imeshuka sana. Nilikuwa naambiwa jana mahindi Ruvuma yamefika shilingi 15,000 kwa gunia, nenda kwenye maeneo yote kwenye mbaazi huko hata sitaki kusema, lakini bidhaa ambazo wananchi wanatakiwa kuuza bidhaa zao wakanunue bidhaa kama sukari, mafuta ya kula na vitu vingine vyote vimepanda sana, sasa uhalisia unakataa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukikubali ni wananchi wangu nikikubali wakulima wa korosho watanishangaa, nikikubali wakulima wa mbaazi, ufuta na wakulima wengine wote katika nchi hii watanishangaa, wakulima wa pamba ambao tumewahasisha wamelima pamba kiasi kile watanishanagaa! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira haya Mheshimiwa Waziri sijui, lakini nilikuwa naangalia Ilani ya Uchaguzi ambayo wengi hawataki tuinukuu, lakini ndiyo tuliyoiombea kura, ndiyo mkataba wetu na wananchi, bajeti hii ukipitia Ilani ya Uchaguzi zinakataana. Sasa kama zinakataana simple logic ndogo tu, tuishauri Serikali irudi mezani, muda upo bajeti kubwa tutakuja kuipitisha baadae, muda upo tuende tukaangalie upya tuweke vipaumbele ndicho tulichokubaliana na wananchi, humu tumekubaliana kwamba wananchi wetu Serikali tutakayoiunda itawasaidia kupata masoko ya nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kelele unazozisikia za mahindi na mazao mengine mgogoro wake uko hapo, kelele unazozisikia za mbaazi mgogoro wake upo hapo, ukimwambia mtu akale magunia 20 ya mbaazi si unamtukana huyu! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Tanzania iliingia mkataba na Serikali ya China tupeleke muhogo, mkataba mmesaini mwezi Mei, 2017 tangazo kutoka Wizarani kwako ya kupeleka imetolewa Aprili. (Makofi)