Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Subhahuna Wataalah.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Waziri Mheshimiwa Dkt. Charles Tizeba aweze kunisikiliza kwa sababu haya ni maagizo ya wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini na Mikoa ya Kusini. Mwaka jana nilichangia Wizara hii kinatoa wasiwasi wangu juu ya suala la usambaji wa magunia na sulphur bure nikaonyesha wasiwasi wangu na yametokea yale yale, kwamba mwaka huu Wizara imesema haitatoa tena sulphur bure na magunia bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka yote kulikuwa na pesa ambazo zilikuwa zinakusanywa ambapo hizi pesa zilikuwa zinapelekwa kwenye Mfuko wa Wakfu, lakini ule mfuko sasa hivi umefutwa na Serikali kwamba zile pesa za export levy taarifa tulizokuwa nazo za msimu wa mwaka jana tumeweza kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 110 ambazo hizo pesa zilitakiwa ziende zikanunue sulphur kwa wananchi wa Mikoa hii ya Kusini, wananchi wanaolima korosho Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zile pesa wakulima wanauliza sana na wameniagiza nije kuzungumza ndani ya Bunge hili kwamba wamekuwa na matatizo makubwa ya sulphur mwaka jana, sulphur badala ya kuzwa shilingi 25,000 zikalanguliwa mpaka shilingi 110,000 kwa mfuko mmoja. Sasa tulikuwa tunaomba sana pesa za service levy ambazo zimekusanywa kupitia kwa wakulima hawa kila kilo moja ya korosho ziko zaidi ya shilingi bilioni 110, tunaomba zinunue pembejeo wakulima hawa, wananchi wa Kusini waweze kupata pembejeo kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hapa kuna wakulima ambao tayari mpaka leo ninavyozungumza wamepeleka pesa zao kwa vyama vya msingi ili waweze kupewa sulphur wengine wametoa shilingi 400,000 wengine shilingi 500,000 lakini mpaka sulphur maeneo mengi haijaenda. Mheshimiwa Waziri hapa amesema kwamba tayari wameagiza sulphur zipo zitaanza kugaiwa Mtwara na Lindi lakini maeneo mengi wananchi wametoa pesa sulphur mpaka leo bado haijafika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la msingi hapa ni kwamba kupulizia korosho wanaanza kuanzia mwezi wa Aprili maeneo mengine mwezi Mei huu, lakini mpaka mwezi wa Juni maeneo yote yanakuwa tayari yameshakamilika. Sasa unaposema sulphur iko njiani mpaka leo hawa wananchi wanaenda kupuliza muda gani. Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana Wizara pesa za service levy, pesa za export levy ambazo zimekusanywa ziende kununua sulphur ziweze kufika kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nimetumwa na wananchi wa Mikoa hii wakulima hawa wa korosho wanauliza suala la CEO ambaye alikuwa anafanya kazi nzuri sana Mheshimiwa Jarufo, tumepata taarifa ambazo siyo rasmi tu kwamba amesimamishwa kazi. Lakini ukaguzi unaonesha huyu jamaa alikuwa anafanya kazi vizuri, anashirikiana na wakulima vizuri, wakulima wanaolima zao hili la korosho, lakini tunaambia tu kwamba ametolewa. Sasa tunaomba majibu ya Mheshimiwa Waziri kwamba kumtoa huyu CEO ni kweli yanayosemwa na wakulima wa korosho kwamba katolewa kwa ajili ya ubaguzi. Tunaomba majibu utakapokuja kutueleza, utueleze kwamba utoaji wa CEO wakulima wa korosho wanasema katolewa kwa ubaguzi, lakini hajafanya jambo lolote baya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilikuwa naomba kuzungumza hapa ni suala la malipo ya korosho. Maeneo mengi mpaka leo ziko zaidi ya shilingi bilioni nne wakulima wa korosho hawajalipwa. Wakulima wanapeleka kwenye vyama vya msingi korosho zao tangu tarehe 17 Novemba, 2017 na naomba ninukuu hapa baadhi ya maeneo tu, kuanzia pale Mtwara Mjini, Tandahimba na maeneo mengine kuna Kata ya Dinduma wananchi wanadai mnada wa tarehe 17 Novemba, 2017 mpaka leo hawajalipwa, wananchi wa Namnyanga, wananchi wa Mdimba, wananchi wa Tumbwe Tarafa ya Namikupa, Tarafa ya Mahuta, Litehu, maeneo haya yote hawajalipwa pesa zao za korosho tangu mwaka jana tarehe 17 Novemba. Jambo hili linaumiza sana kwa kweli wakulima wanajitahidi kulima kwa muda mrefu, wanalima wanapata changamoto nyingi, lakini pesa zao hawapewi kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala hili la AMCOS, wanaoteuliwa kuingia kwenye AMCOS hizi wanakuwa ni watu ambao hawana uwezo, ni watu ambao wanaenda pale kwa uwakilishi wa wananchi bila kufuata vigezo na wahasibu ambao wanaingia kwenye hivi vyama vya msingi wanakuwa ni wajanja sana, wanapiga mabilioni ya pesa sana wahasibu kwa sababu viongozi wa AMCOS hawana elimu uwezo wao ni mdogo.

Naomba Mheshimiwa Waziri ulete muswada tubadilishe sheria hapa kwamba kila aneyeajiriwa kwenye AMCOS hizi, kila anayegombea kwenye AMCOS kuwe na sifa fulani angalau ya elimu wanapigwa sana, wakulima wanaibiwa sana Wahasibu wa hizi AMCOS zote kwa sababu uwezo wao ni mdogo. Kwa hiyo, naomba tulete Muswada wa Sheria kubadilisha hizi sheria waajiriwa waweze kuwa na uwezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine Mheshimiwa Waziri hapa wakati anazungumza ameleza kwamba kuna Tume ya kusimamia kilimo kule maeneo ya Kusini nami nilikuwa naomba sana kwa sababu maeneo ya Kusini ni asilimia 90 ya ardhi ni ardhi ambayo inarutuba sana.