Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kutokana na muda mfupi nitaenda moja kwa moja kwenye suala la mbolea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, rejea ukurasa wa 41 wa kitabu hiki cha bajeti ya Wizara. Utafiti wa udongo unaonesha kuwa mbolea inayofaa karibu kwa kanda nyingi zinazolima mahindi na nafaka nyingine ni Nitrogen Phospharus Sulphur (NPS) na NPS Zinki. Huo ndiyo utafiti aliotuletea kwenye bajeti yake Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kwenye ukurasa wa 26 Mheshimiwa Waziri anatuambia kuwa mbolea ambayo inaagizwa kwa pamoja (Bulk Procurement System) ni mbolea ya DAP na Urea. Sasa kitaalam maana yake nini? Tunasisitiza tufanye utafiti, wakulima walime kwa tija, sasa wewe unang’anga’ania DAP na Urea kwa sababu tumeizoea. DAP ni kwa ajili ya mizizi na Urea inatengenezwa kutokana na zao la petroli, asilimia 70 ukiiweka inayeyuka, inapotea. Sasa mnatulepeka wapi? Kwa kweli hivi ndiyo vitu nafikiri Waziri alipotoka kidogo tu labda akija kesho ajaribu kutuambia kwa nini hafuati utafiti unavyosema? (Makofi)

Mheshmiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ningependa kulisemea ni kahawa. Uzalishaji wa kahawa unapungua mwaka hadi mwaka. Tulikuwa na tani 61,000 mwaka 2015/2016 zikapungua kuja tani 48,000, zikapungua mwaka jana kuja tani 36,000 na sasa hivi kuna projections kidogo na tulitegemea kwamba zitafika tani 100,000. Tatizo nalo liko wapi hapa? Tatizo lipo kwenye usimamizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la kahawa linasimamiwa na TCB. Nikiangalia muundo wa TCB mpaka leo nashindwa kuuelewa. Kwa sababu TCB alitakiwa kuwa regulator lakini vilevile ndiye anayehusika na masoko. Mnada wa kahawa unasimamiwa na TCB, kwa kiasi kikubwa wakulima wananyonywa sana. Leo hii mnada wa kahawa ya Tanzania arabica ni dola 3 kwa kilo, kwa Kenya jirani zetu kahawa hiyo hiyo ya arabica ni kati ya dola 7 -10, angalia tofauti hiyo. Ukienda Ethiopia bei inakuwa ni nzuri zaidi, ni kwa nini? Kwa sababu huwezi ukamuweka regulator mtu mmoja huyo anasimamia uuzaji wa kahawa na pale bei hazipangwi kwenye mnada, watu wanakubaliana nje ya mnada. Wakienda pale ni kuthibitisha tu kwamba hii kahawa tunatainunua kwa dola, anayenyonywa ni nani? Anayenyonywa ni mkulima na ndiyo sababu wakulima hataki kuendelea tena na kulima kahawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kununua mbolea, achilia mazao mengine, kwa sasa hivi ukilima mahindi huwezi kununua ambolea. Kwa hiyo, tukisema kuwa tunaongeza mazao, tunaongeza uzalishaji, tunaongeza productivity, sasa hivi huu mfumo tulio nao ukilinganisha masoko na uzalishaji haviendi pamoja. Leo mfuko wa mbolea kwa ajili ya kahawa ni zaidi ya Sh.70,000 unahitaji mifuko mitatu, ukiuza kwa dola 3,000 huwezi tena kulihudumia hilo shamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna chombo kipya cha bidhaa za mazao (Tanzania Commodity Exchange Market), hiyo ndiyo tuifuate. Inafanya vizuri Nairobi na Ethiopia, itaweka bei wazi. Vilevile hata ukwasi (liquitidy) kwa ajili ya wakulima itakuwa nzuri. TCB tunalipa baada ya wiki mbili lakini nina imani kwa Sheria ya Tanzania Commodity Exchange Market ni siku moja, wanaita T+1, siku ya pili unalipwa hela yako. Sasa hizi siku 14 zile hela zikikaa TCB ni nani anayefaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo wakulima wananyonywa sana ni kwamba kahawa tunauza kwa forex na halmashauri zetu ile service levy nayo anakatwa mkulima kwa forex lakini exchange rate inayotumiwa na TCB wanaamua wenyewe, ni pesa nyingi sana inayopotea. Naomba Wizara au Serikali kwa ujumla ielekeze kwamba haya mazao yote, iwe nafaka, korosho, kahawa ziende kwenye soko la bidhaa, ndivyo duniani kote biashara za namna hiyo ndiko zinakokwenda huko. Huku tulikozoea huku, ushirika ndiyo nakubaliana wakusanye wapeleke sokoni, lakini sokoni kule ziuzwe kisasa na chombo hicho tunacho, tukitumie.