Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Kilimo

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja hii ya Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania. Ripoti ya CAG ya mwaka 2016/ 2017 inaonyesha kuwa kiasi kikubwa cha fedha kinawekwa amana ya kudumu. Kwa mwaka 2016/2017, inaonyesha kwamba fedha zilizowekwa amana ni shilingi bilioni 54.7. Badala ya kutoa mikopo kwa wakulima fedha inakwenda kuwekwa kwenye amana na shughuli kubwa ya benki hiyo ilikuwa ni kuwasaidia wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2016/2017, benki hiyo imetoa shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya watumishi. Kwa hiyo, kiasi kidogo ambacho kilitolewa mkopo kwa ajili ya sekta ya kilimo, shilingi bilioni 2.2 tu. Vilevile benki hiyo imekuwa maeneo ya mjini tu na hasa Dar es Salaam. Waziri atueleze ni kwa nini benki hiyo haiendi mikoani na hatimaye wilayani na vijijini? Naomba kuishauri Serikali ifanye haraka sana kuhakikisha benki hiyo inafika huko chini kwa wakulima. Kwa sababu Dar es Salaam hakuna wakulima kule, wakulima wako huko vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo napenda kuchangia ni upatikanaji wa pembejeo kwa wakati. Mwaka jana tualiahidiwa hapa Bungeni kwamba mbolea zitafika kwa wakati na kwa bei nafuu lakini cha kushangaza wakulima wetu wamepata shida sana, kuanzia mwaka jana Oktoba walipoanza kufanya shughuli za kilimo mbolea ikachelewa na Januari hapakuwepo mbolea ya kukuzia. Kama kweli tunataka kwenda kwenye Tanzania ya viwanda, tunaendaje kama hatutekelezi yale ambayo tunawaahidi wananchi wetu? Mheshimiwa Waziri kwa kweli inasikitisha wananchi wetu mwaka huu wamekata tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee pia suala la ukosefu wa soko. Wananchi wetu pamoja changamoto walizo nazo wamehamasika, wamelima kwa wingi lakini hakuna soko, mazao yote hakuna soko. Katika Mkoa wangu wa Njombe tunalima kwa wingi mahindi, viazi na matunda lakini hivyo vyote havina soko. Kwa mfano, mwaka 2016/ 2017 tumezalisha mahindi tani 571,000 na matumizi yanatakiwa tani 172,000 hivyo kuwa na ziada tani 399,000. Inasikitisha, baada ya kuzalisha kwa wingi namna hiyo wananchi hawa walitakiwa wapate faraja, wapate fedha za kuweza kusomeshea watoto wao lakini wakazuiliwa wasipeleke mahindi haya nje. Kwa kweli inasikitisha, inasikitisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha hoja yake atueleze wananchi hawa watafanya nini na mahindi hayo? Maana sasa hivi tunaingia kwenye msimu mwingine, mahindi sasa hivi yamestawi nchi nzima, je, tutafanyaje na mahindi hayo? Naomba tuone ni namna gani tunawahurumia hawa wananchi ambao wanatumia gharama kubwa kununua pembejeo lakini mwisho wa siku wanakuja kuuza debe moja Sh.3,000 au Sh.2,000 kwa kweli inasikitisha.