Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kuchangia hoja iliyoko mezani. Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania limejijengea heshima kubwa ndani na nje ya nchi. Hata hivyo, kwa miaka hii ya karibuni tumeshuhudia wanasiasa hasa viongozi wakijihusisha kwenye mambo ya siasa, kwa mfano, Kamisheni ya Kijeshi kupokea Madiwani waliohama chama; na Wanajeshi kuwepo barabarani kuogopesha wananchi wasiandamane ilhali jukumu hilo ni la Polisi.

Mheshimiwa Spika, kuna usemi, “vyombo vya ulinzi na usalama wakilinda dola, wanakuwa adui wa wananchi”. Jeshi letu lilijengewa heshima kubwa ya kulinda mipaka yetu, hivyo liepuke kwa nguvu zote kuhusishwa na mambo ya siasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Jeshi liangaliwe upya kwa makini ili kuepuka vijana watakaotia doa Jeshi la Wananchi. Baada ya kumaliza mafunzo ya JKT, kabla ya kuajiriwa wafanyiwe psychometric test ili kubaini vijana wenye tabia na maadili ambayo hayakidhi maadili na nidhamu ya Jeshi. Kwa kutumia tool hiyo, Jeshi litafanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa vijana wenye tabia mbaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.